Jumapili, 30 Machi 2014

29% WANAUME WANAMAHUSIANO NJE YA NDOA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa 29/03/2014
Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Zaidi ya 5% ya wanandoa wameambukizwa maambukizi ya virusi vya Ukimwi nchini wakati asilimia 29 ya wanaume wanakadiriwa kuwa na mahusiano nje ya ndoa.
 
Simon Keraryo
Kauli hiyo imetolawa na Simon Keraryo, kutoka TACAIDS alipokuwa aliwasilisha mada juu ya mwenendo wa Ukimwi nchini katika "Media Orientation" iliyofanyika katika hoteli ya Kalenga West Park mjini Iringa.
Keraryo amesema kuwa pamoja na kushuka kwa maambukizi ya Ukimwi, bado kuna changamoto kubwa katika udhibiti wa Ukimwi nchini katika maambukizi mapya. Amesema kuwa inakadiriwa zaidi ya watu 100,000 wanaambukizwa Ukimwi kila mwaka.

Amesema kuwa hali hio inasababishwa na tabia zenye kuchangia maambukizi. Akitolea mfano mwaka 2008 asilimia 18 ya wanaume na asilimia tatu ya wanawake waliripotiwa kuwa na wapenzi zaidi ya mmoja nchini.  Amesema kuwa kiwango hicho kimeongezeka hadi kufikia 21% ya wanaume na asilimia nne kwa wanawake 2012.

Kuhusu uhusiano nje ya ndoa, Keraryo amesema kuwa 29% ya wanaume na 16% ya wanawake wanakadiriwa kuwa na mahusiano nje ya ndoa. Ameongeza kuwa inakadiriwa kuwa asilimia 5.3 ya wanandoa wameambukizwa virusi vya Ukimwi.

Akiongelea hali ya maambuki ya Ukimwi nchini, Keraryo amesema kuwa kiwango cha ushamiri wa VVU kimeshuka kutoka asilimia 7 mwaka 2003/2004 hadi kufikia asilimia 5.3 mwaka 2011/2012. Amesema kuwa kiwango cha maambukizi kimeshuka kwa wanaume kutoka asilimia 6.3 mwaka 2003/2004 hadi kufikia asilimia 3.9 mwaka 2011/2012.

Akiongelea maambukizi kwa makundi maalumu, amesema kuwa maambukizi ni makubwa kwa wauza ngono na wateja wao kufikia 31.4%.  amesema kuwa wanaume wanaofanya ngono wao kwa wao ni 41% na 34.8% watu wanaojidunga dawa.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...