Alhamisi, 27 Machi 2014

SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI YAUA WANAWAKE WENGI NCHINI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

ASILIMIA kubwa ya wanawake wa Tanzania ni wahanga wa saratani ya mlango wa kizazi ikichangia vifo vingi kutokana na wagonjwa wanaogundulika na ugonjwa huu wakiwa katika hatua isiyotibika.
 
Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu
Kauli hiyo imetolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu alipokuwa akizindua mradi wa kuhamasisha jamii kuhusu huduma za uchunguzi wa saratani ya shingo ya kizazi uliofanyika katika ukumbi wa chuo cha Veta mjini Iringa.

Amesema “Tanzania ni mojawapo ya nchi zinazokumbwa na mzigo mkubwa wa saratani ya shingo ya kizazi duniani. Asilimia 25% ya wanawake wa Tanzania wako hatarini kupata saratani ya mlango wa kizazi katika maisha yao, saratani hii ni mojawapo ya sababu kubwa zinazosababisha vifo vya wanawake nchini”. Amesema kuwa asilimia 80 ya wagonjwa wanaogundulika na aina hiyo ya saratani hugundulika katika hatua kubwa ya ugonjwa ambapo hakuna tiba wala kinga.

Akiongelea takwimu kutoka taasisi ya saratani ya Ocean road, amesema kuwa takwimu hizo zinaonesha kuwa kati ya wagonjwa wa saratani wanaopelekwa katika taasisi hiyo kila mwaka, zaidi ya wagonjwa 5,000 wana tatizo la saratani ya mlango wa kikazi. Amesema kuwa serikali kupitia wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inafanya juhudi mbalimbali katika kupambana na saratani ya mlango wa kizazi kwa wanawake. Amesema kuwa saratani ya mlango wa kizazi inatibika pale inapogundulika katika hatua za awali.

Katibu Tawala Mkoa wa Iringa amesema kuwa upo uhusiano mkubwa kati ya saratani ya mlango wa kizazi na maambukizi ya virusi vya Ukimwi. Amesema kuwa takwimu za utafiti wa viashiria vya Ukimwi na Malaria nchini zinaonesha kuwa na kiwango kikubwa cha maambukizi ya virusi vya Ukimwi kwa asilimia 9. Amesema kuwa takwimu hiyo inatoa picha ya ukubwa wa tatizo la saratani ya mlango wa kizazi kwa mkoa wa Iringa. Amesema kuwa kutokana na ukubwa wa tatizo hilo, wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii peke yake haiwezi kutatua tatizo la saratani ya mlango wa kizazi. Ametoa wito kwa wadau mbalimbali kuunga mkono ili kuhakikisha kuwa akina mama na kina dada wako salama dhidi ya tatizo hilo.
 
Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa T-MARC TANZANIA Diana Kisaka
Aidha, ametoa wito kwa wanawake na wasichana kujitokeza kwa wingi ili kufaidika na huduma za uchunguzi wa awali zitakazotolewa katika vituo mbalimbali vya afya mkoani Iringa. Vilevile, amewataka wanaume kuwahamasisha akina mama na mabinti ili waweze kujitokeza kwa wingi kupatiwa elimu na huduma ya uchunguzi itakayotolewa bure.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...