Alhamisi, 27 Machi 2014

WAKAZI 2379 KUPATA MAJI SAFI NA SALAMA KILOLO



Zainab Maeda.
Iringa,
WAKAZI wapatao 2379 wa kijiji cha Ikuka katika halmashauri ya wilaya ya Kilolo mkoani Iringa ambao walikuwa wanalazimika kutembea umbali mrefu kupata huduma ya maji safi na salama toka Uhuru wa Taifa hili sasa wanatarajia kupata huduma hiyo baada ya kukamilika  kwa mradiu mkubwa wa maji kijijini hapo.

Akisoma taarifa ya mradi huo  mhandisi wa maji wilaya ya Kilolo katika siku ya maadhimisho ya kilele cha wiki ya maji , Enock Basyegile alisema kuwa wakazi wa kijiji hicho wanatarajia kupata huduma hiyo ya maji safi na salama endapo mradi huo utakamilika kwa wakati.

Alisema kuwa mradi huo  umegharimu zaidi ya milioni 400 unatarajiwa kumalizika juni 30 mwaka huu ambapo bado kiasi cha fedha zaidi ya shilingi milioni 11 ilii kukamilika kwa mradi
Alisema kuwa mradi huu unatekelezwa chini  chini ya miradi ya Matokeo Makubwa sasa (BRN).

“Mradi huu ulianza juni 26 mwaka 2013 na unatarajia kuwa mradi huu utakamilika juni 30 mwaka huu,ili kukamilika kwa mradi huu zaidi ya shilingi 11 milioni zinahitajika ili wananchi waweze kupata huduma hii kwa wakati unaotakiwa”Alisema Basyegile.

Naye mwakilishi wa mkuu wa mkoa wa Iringa wakati akizindua mradi huo Gerald Guninita aliwataka wakazi wa kijiji hicho kuutunza mradi huo ili uwe endelevu.

Guninita ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Kilolo alisema kuwa jukumu la kulinda mradi huo ni la wananchi wenyewe ambao ndio walengwa wa matumizi ya maji safi na salama.

“Wakazi wa kijiji cha Ikuka mnatakiwa kuutunza mradi huu ikiwa ni pamoja na kuyatunza mazingira na vyanzo vya maji ili muweze kunufaika na kuufanya mradi kuwa endelevu”alisema Guninita na kuongeza kuwa.

“Sheria na hatua zitachukuliwa kwa atakaebainika kufanya uharibifu wa mradi huo kama vile wizi wa mambomba na vinginevyo vilivyopo katika mradi”

Wananchi wanaopata huduma ya maji safi na salama mijini katika mkoa wa Iringa ni 189,644 kati ya wananchi 247,156 ambao ni sawa na asilimia 76.7 ya wananchi waishio mijini.

Hali ya huduma ya maji mijini inategemewa kuongezeka mara baada ya kutekelezwa kwa miradikatika miji ya Ilula,Kilolo,na Mafinga,na miradi hii inategemewa kutekelezwa kupitia program ya maendeleo ya sekta ya maji (WSDP) ambapo jumla ya wananchi 57,512 watapata huduma bora ya majisafi na salama.
Mwisho.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...