Ijumaa, 2 Mei 2014

WADAU WATAKIWA KUHAMASISHA CHANJO YA SURUA


VIONGOZI wa dini, watumishi wa serikali na waandishi wa habari mkoani Iringa wametakiwa kusaidia katika kuhamasisha, zoezi la chanjo ya surua dozi, ya pili inayotarajiwa kuanza mei mosi, ikiwahusisha watoto wenye umri wa miezi 18.
 
Rai hiyo imetolewa leo mkoani Iringa, wakati wa mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa wa katibu tawala, mkoani Iringa.
Akitoa mafunzo hayo, Mratibu wa afya ya uzazi na mtoto mkoani Iringa, Mariam Mohamed amesema mbali na mafunzo kwa makundi hayo tayari, wamefanikiwa kutoa mafunzo kwa wajumbe wa kamati za afya za vijiji, mitaa na kata na wilaya ili kuongeza uelewa juu ya chanjo hiyo.
 
Aliitaka jamii kuondoa dhana finyu kuhusiana na chanjo, kwa madai kuwa lengo la zoezi hilo ni kuendelea kupambana na virusi vinavyosababisha ugonjwa wa surua ambao hivi sasa ni tishio kwa watoto.
 
“Surua ni ugonjwa hatari unaosababishwa na virusi vya surua hivyo chanjoa ya surua ni muhimu kwa watoto kwani  inaubora uliothibitishwa na wizara ya afya na ustawi wa jamii na shirika la afya ulimwenguni..ni salama,” alisema..
 
Aliwataka wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ili waweze kupatiwa chanjo hiyo.
@MUITIKIO BLOG


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...