Jumatano, 18 Juni 2014

IRINGA WATAKIWA KUWAACHIA WATOTO WAO KWENDA SHULE



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Wazazi mkoani Iringa wameaswa tabia ya kuwaficha watoto wao wanapofikia umri wa kuanza shule na kuwaandaa kwa lengo la kufanya kazi za majumbani na kuolewa.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na mkuu wa wilaya ya Iringa, Dkt. Leticia Warioba katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa afrika yaliyofanyika ngazi ya mkoa katika kijiji cha Tanangozi wilayani Iringa.
Dkt. Ishengoma amesema kuwa ipo tabia ya baadhi ya wazazi kuwaficha watoto wao wanapofikia umri wa kwenda shule na kuwaandaa kwa lengo la kufanya kazi za majumbani ama kuolewa. Amesema kuwa wazazi na walezi huwasafirisha watoto wao kwenda katika miji mikubwa kwa lengo la kufanya kazi za majumbani. Amewataka wazazi kuacha tabia hiyo inayopelekea watoto kuishi katika mazingira hatarishi. Amezitaka familia zote kuhakikisha watoto wanapata elimu iliyo bora na isiyo na vikwazo. Akiongelea kaulimbiu, mkuu wa Mkoa amesema kuwa mwaka 2014 kaulimbiu ya maadhimisho ni “kupata elimu bora na isiyo na vikwazo ni haki ya kila mtoto”. Ameitaja kauli mbiu hiyo kuwa inayohimiza jamii mzima kufuata maelekezo ya sheria namba 2 ya mtoto ya mwaka 2009 pamoja na sheria ya elimu ya mwaka 1978 vyombo ambavyo ndivyo miongozo ya kuhakikisha watoto wanapata haki za msingi ikiwa ni pamoja na elimu.
Mkuu wa mkoa ameitaka jamii kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha na kuimarisha miundombinu iliyopo shuleni kwa kuchangia ujenzi wa nyumba bora za walimu na za kutosha, kuongeza idadi ya madawati ili watoto wasikae chini, kuboresha hali ya usafi wa mazingira ikiwepo idadi ya matundu ya vyoo kwa wasichana na wavulana, upatikanaji chakula cha mchana kwa watoto wanapokuwa shuleni.

  






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...