Jumapili, 29 Juni 2014

VIJANA WAWEKEZE ...



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Vijana nchini wametakiwa kuwekeza katika miradi ya utunzaji wa mazingira ili taifa liweze kuwa mahali salama kwa kizazi kilichopo na vizazi vijavyo.
Kauli hiyo imetolewa kiongozi wa wakimbiza Mwenge wa Uhuru mwaka 2014 Rachel Kassanda baada ya kuzindua mradi wa hifadhi ya mazingira na kukagua mradi wa ufugaji wa nyuki wa vijana na kutundika mizinga katika kijiji cha kinyanambo ‘C’ wilayani Mufindi.
Kassanda amesema kuwa umefika wakati kwa vijana nchini kubuni miradi ya utunzaji wa mazingira. Amesema kuwa miradi ya utunzaji wa mazingira na ufugaji nyuki ni miradi yenye tija kwa muda mrefu kwa vijana na kwa taifa kwa ujumla. Amewapongeza vijana hao kwa kubuni miradi hiyo inayowawezesha kujiongezea kipato na kutunza mazingira.
Katika taarifa fupi ya mradi wa hifadhi ya mazingira na ufugaji nyuki wa vijana imetaarifiwa kuwa lengo la mradi huo wa upandaji miti na ufugaji nyuki ni kuhifadhi mazingira na kuwekeza katika sekta ya misitu na nyuki ili kuweza kujikwamua kiuchumi.
Akiongelea gharama katibu wa kikundi Violeth Matala amesema kuwa miradi yote ya upandaji wa miti na ufugaji wa nyuki imegharimu shilingi 48,333,330. Ameutaja mchanganuo wake kuwa ni mradi wa upandaji miti shilingi 45,683,330 kwa lengo la kukunua ardhi, upandaji na gharama za utunzaji. Amesema kuwa mradi wa ufugaji nyuki shilingi 2,650,000 kwa ajili ya ununuzi wa mizinga usharifishaji na utunzaji wa shamba. Amesema kuwa halmashauri ya wilaya imechangia shilingi 500,000/= kwa ununuzi wa mizinga ya kisasa.
Shamba hilo lina hekari 20 lililopandwa mikaratusi likiwa na mizinga 55 hadi sasa.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...