Jumapili, 29 Juni 2014

KIONGOZIN WA MBIO ZA MWENGE RACHEL WA UHOLANZI AFUNGUKA...



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Rachel Kassanda amewapongeza wakinamama wa kikundi cha Tuinuane kwa kazi za kujiongezea kipato na kukabiliana na umasikini.
Kassanda ameyasema hayo alipokuwa akizindua kikundi hicho na kukabidhi hundi ya shilingi 1,000,000 ukiwa ni mchango kutoka halmashauri ya wilaya ya Iringa kwa lengo la kukiongezea mtaji kikundi hicho ili kiweze kujitegemea.
Amepongeza juhudi za kujiongezea kipato kupitia utaratibu wa hisa ambapo wanachana waliweza kukusanya kiasi cha shilingi 240,000 na kujiunga na Mazombe SACCOS hatimaye kupata mkopo wa shilingi 4,400,000.
Akiwasilisha taarifa ya kikundi cha wanawake Tuinuane, Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Masukanzi Jumanne Tembo amesema kuwa kikundi hicho kilianza mwaka 2012 kikiwa na wanachama 23. Amesema kuwa kikundi hicho kilianzishwa kwa lengo la kuwaongezea kipato wanakikundi.
Tembo amesema kuwa kikundi hicho kimefaidika na mradi wa Corridor Economic Empowerment Project (CEEP) kuwapatia elimu ya kujikinga na maambukizi ya VVU.
=30=




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...