Alhamisi, 17 Julai 2014

RC IRINGA AFUTURISHA IKULU



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma amefutarisha wananchi kwa lengo la kujenga umoja na kuaminiana ili kudumisha amani na utulivu.
 
Muda wa futari wanaume

Futari kwa akina mama

Kauli hiyo ameitoa alipokuwa akiongea na waumini wa dini ya kiislamu na wananchi kwa ujumla waliohudhuria futari hiyo katika viwanja vya Ikulu ndogo iliyopo mjini Iringa. Amesema “lengo la kuandaa futari hii ni kutuweka pamoja kwa lengo la kujenga na kudumisha umoja wetu”.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa amewataka viongozi wote wa dini kutumia muda wao kuuombea Mkoa wa Iringa na Taifa kwa ujumla ili amani ya kudumu iendelee kushamiri nchini.
Akiongelea wajumbe wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), Dkt. Ishengoma amesema kuwa hata wale wasiotaka kurudi bungeni waombewe ili waweze kurudi bungeni. Amesema kuwa tofauti na kutokuelewana kunatatuliwa kupitia vikao na meza ya majadiliano.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...