Alhamisi, 17 Julai 2014

WILAYA ZITATUE TATIZO LA AJIRA KWA VIJANA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Wilaya zimetakiwa kubuni mipango ya kutatua tatizo la ajira kwa vijana ili waweze kujiajiri na kujiletea maendeleo.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma alipokuwa akikabidhiwa mashine 16 za kufyatulia matofali kutoka shirika la nyumba la Taifa (NHC) katika uwanja wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Iringa. 
 
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. christine Ishengoma akipokea mashine za kutengeneza tofali toka kwa Meneja wa NHC Iringa
Dkt. Ishengoma amesema “natumia fursa hii kutoa wito kwa wilaya na halmashauri zote kubuni mipango ambayo itawezesha kutatua tatizo la ajira kwa vijana kwa haraka kama ilivyo kwa mradi huu wa kufyatua tofali”. Amewataka msaada huo uliotolewa uwe ni changamoto kwao kuendelea kuunda vikundi vya uzalishaji mali vya vijana nan kutenga fedha zaidi kwa ajili ya kusaidia miradi ya maendeleo ya vijana. Aidha, amezitaka halmashauri kuongeza vikundi vingi na kuwanunulia vijana mashine za kutengenezea matofali na kuvikopesha vikundi hivyo kwa lengo la kuvifanya endelevu.
Akiongelea vijana waliochaguliwa kupata msaada wa mafunzo na mashine hizo 16, Mkuu wa Mkoa wa Iringa amewataka vijana hao kuzitunza vizuri mashine hizo kama mafunzo waliyopewa. Amesema kuwa serikali inategemea kuona hali za kimaisha za vijana hao zinabadilika na kuwa bora sambamba na vikundi kuimarika. Amewataka kutumia fursa hiyo ya kupewa mashine hizo kama chachu ya kuonesha uwezo na ubunifu zaidi. Amesema kuwa kufanya kwao vizuri kutawafanya vijana wengine kwenda kujifunza kwao kwa lengo la kuwa na uelewa mpana.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...