Jumanne, 1 Julai 2014

UKAWA WARUDI BUNGENI- NIWEMUGIZI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Baraza la Maaskofu Katoliki limewataka wajumbe wa umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA) kurejea bunguni bila masharti ili kuhakikisha mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya unafanikiwa.
Kauli hiyo imetolewa na Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Tanzania Askofu Severine Niwemugizi katika hotuba yake baada ya misa takatifu ya sherehe ya jubilei ya miaka 25 ya uaskofu wa Mhashamu Tarcisius JM. Ngalalekumtwa iliyofanyika katika kanisa katoliki la Kihesa.
Severine Niwemugizi, Makamu Mwenyekiti wa TEC
 Askofu Niwemugizi amewataka wajumbe wote wanaounda umoja wa katiba ya wananchi kurudi bungeni mwezi ujao pasipo masharti yoyote. Amesema kuwa wajumbe hao warudi bungeni na kujadili rasimu ya pili ya katiba mpya kwa mujibu wa sheria. Amesema kuwa jukumu hilo ndilo walilotumwa kwa mujibu wa sheria. Aidha, amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la wapiga kura.
Katika hotuba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda amesema kuwa serikali itaendelea kuthamini na kuunga mkono mchango wa taasisi za kidini katika kuleta maendeleo nchini. Amesema kuwa taasisi za kidini zimekuwa zikichangia kwa kiasi kikubwa katika ukuaji na uboreshaji wa huduma katika nyanja za elimu, afya malezi na mambo mengine kama hayo.
Akiwatambulisha wageni waliohudhuria misa ya jubilei, mkuu wa mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma amesema kuwa mkoa wa Iringa unautulivu na usalama wa kutosha. Amesema kuwa mkoa unajivunia ukarimu wa wananchi wake jambo litakalowafanya wageni kufurahia uwepo wao mkoani Iringa.
 
Waziri Mkuu Mizengo Pinda
Amempongeza baba Askofu Ngalalekumtwa kwa kutimiza miaka 25 ya uaskofu na kumtakia maisha marefu zaidi ili aendelee kuwahudumia watanzania kiroho.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...