Jumapili, 13 Julai 2014

ZAIDI YA 24% PATO LA TAIFA NI KILIMO

NA. OFISI YA MKUU WA MKOA



Sekta ya kilimo inayochangia zaidi ya asilimia 24 ya pato la taifa imejizatiti kupitia mpango wa matokeo makubwa sasa kuongeza uzalishaji wa mahindi na mpunga ili kuwa na uhakika wa usalama wa chakula na kuuza nje ya nchi.
Kauli hiyo imetolewa na waziri wa kilimo, chakula na ushirika, Mhandisi. Christiper Chiza alipokuwa akihutubia wananchi na wadau wa sekta hiyo katika siku maalum ya mpango wa matokeo makubwa sasa (BRN) katika kilimo iliyotolewa kituo cha mafunzo ya wakulima Mkindo, wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro.
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mhandisi. Christopher Chiza
Mhandisi. Chiza amesema “sekta ya kilimo inachangia kwa asilimia 24.5 ya pato la Taifa; inachangia zaidi ya asilimia 100 ya mahitaji ya chakula nchini; inatoa ajira kwa wastani wa asilimia 74 ya watanzania; inachangia kwa asilimia 33 ya fedha za kigeni; na ni chanzo kikubwa cha malighafi kwa viwanda vyetu vya ndani”.
Amesema kuwa hadi kufikia mwaka 2016, mpango wa matokeo makubwa sasa utafanikisha ongezeko kwa uzalishaji wa mahindi kwa tani 100,000 kutoka tani milioni 3.4 kwa mwaka. Amesema kuwa sekta inalenga ongezeko la kuzalisha mpunga kwa tani 290,000 kutoka tani milioni 1.3 zinazozalishwa sasa.
Maeneo mengine ameyataja kuwa ni pamoja na kuendeleza eneo jipya la kilimo cha kibiashara hekta 350,000 na kuboresha eneo la wakulima wadogo hekta 330,000. Maeneo mengine ni kuongeza uzalishaji wa sukari kwa tani 150,000 na kuongeza idadi ya wakulima watakaoshiriki kuwa zaidi ya 400,000.
Waziri wa kilimo, chakula na ushirika amesema kuwa utekelezaji wa mpango wa matokeo makubwa sasa kwa mwaka 2014/ 2015 utakuwa katika maeneo ya kuendeleza mashamba 8 ya kilimo cha kibiashara cha miwa na mpunga. Eneo lingine amelitaja kuwa ni kuboresha skimu 39 za umwagiliaji mpunga kwa kujenga miundo mbinu ya umwagiliaji na maghala kwa ajili ya uhifadhi wa mpunga ili kurahisisha upatikanaji wa masoko na kuboresha maghala 145 kwa ajili ya uhifadhi wa mahindi ili kurahisisha upatikanaji wa masoko.
Mwakilishi wa mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya bunge ya Kilimo, Maji na Mifugo, Dkt. Christine Ishengoma ambaye pia ni mkuu wa mkoa wa Iringa amesema kuwa umefika wakati kwa vijana kujikita katika shughuli za kilimo nchini. Amesema kuwa kamati yake itaendelea kushauri kuboreshwa kwa mazingira mazuri katika sekta ya kilimo ili kuwavutia vijana wengi kujikita katika sekta ya kilimo. Amesema kuwa mazingira mazuri yatachangia ajira kwa vijana na kukuza pato la kaya na taifa kwa ujumla. 
Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Kilimo, Maji na Mifugo Dkt. Chhristine Ishengoma (Mb.)
Rozina Mkude ambaye ni mkulima wa mpunga katika kijiji cha mkindo wilayani Mvomero amepongeza jihudi za serikali kukuza sekta ya kilimo nchini. Amesema mpango wa sasa wa kukifanya kilimo kiwe cha kibiashara utasaidia kukuza kipato cha familia na kuondoa umasikini kupitia sekta ya kilimo. Amesema kuwa ni mara ya kwanza kwa sehere hizo kufanyika kijijini na kuwahusisha wananchi wengi ambao ndio wakulima halisi tofauti na wakulima wa vitabuni.
Sekta ya kilimo inakuwa kwa wastani wa asilimia nne kwa muongo mmoja sasa ikiongozwa na kaulimbiu isemayo matokeo makubwa sasa, kilimo ni biashara.
Mashine ya Mpunga

=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...