Jumanne, 23 Desemba 2014

IRINGA YAPATA KIBALI CHA KUENDELEZA BOMA LA MJERUMANI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Mkoa wa Iringa umepata kibali cha kumiliki na kuendeleza jengo la kale lililojengwa na utawala wa kijerumani maarufu kama Iringa Boma.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu ukaratabi wa wa jengo la zamani la ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Iringa ambalo litakuwa makumbusho ya Mkoa baada ya kukamilika. Taarifa hiyo ilitolewa katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa. 
Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu
Wamoja amesema “nimefurahi sana kwa kupata fursa hii adhimu kutangaza rasmi kuwa mkoa wetu umepata kibali kilichongojewa kwa muda mrefu cha kumiliki na kuendeleza jengo la kale lililojengwa na utawala wa kijerumani lenye umri wa miaka 114, maarufu kama Iringa Boma.” Amesema kuwa kibali hicho kimetolewa na wizara ya maliasili na utalii. 

Amesema kuwa lengo ni kulibadilijengo hilo na kulitumia kama jumba la makumbusho. Amesema kuwa watakusanya na kuweka kumbukumbu, kufanya maonesho mbalimbali ya urithi na utamaduni wa Mkoa wa Iringa kwa lengo la kukuza utalii na kuleta maendeleo endelevu. “urithi wetu na utamaduni wetu ni uti wa mgongo wa utambulisho wetu kama wanadamu. Kuwepo kwa lugha anuai, tamaduni, dini, muziki pamoja na ala mbalimbali za muziki, kazi za sanaa na jinsi tunavyoishi inaashiria na kuthibitisha dhahiri urithi wa mila zetu mbalimbali.” Alisisitiza Wamoja.
Iringa Boma
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...