Jumanne, 23 Desemba 2014

UFAULU WAONGEZEKA MATOKEO YA DARASA LA SABA IRINGA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Matokeo ya ufaulu kwa mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2014 ni mazuri ikilinganishwa na mwaka 2013 pamoja na Mkoa wa Iringa kushika nafasi ya nne kitaifa.

Kauli hiyo imetolewa na Afisa elimu wa Mkoa wa Iringa, Mwl. Joseph Mnyikambi alipokuwa akiwasilisha Taarifa ya mwelekeo wa matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2014 kwa Mkoa wa Iringa katika kikao cha uchaguzi wa wanafunzi wa kujiunga na kidato cha kwanza katika Mkoa wa Iringa kilichofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa.
Mwl. Mnyikambi amesema, “Matokeo kwa ujumla kimkoa ni mazuri. Kiwango cha ufaulu kimepanda kwa Halmashauri zote.” 
Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu (kulia) na Afisa Elimu Mkoa wa Iringa, Mwl. Joseph Mnyikambi (kushoto

Akiongelea hali ya matokeo kimkoa, amesema kuwa jumla ya shule za msingi 458 zenye watahiniwa 21,363 walifanya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi mwaka 2014. Amesema kuwa hali ya ufaulu imeongezeka katika halmashauri ikilinganishwa na mwaka 2013. Iringa (M) ufaulu umeongezeka 0.59%, Iringa 5.97%, Kilolo 03%, na Mufindi 4.31%. 

Afisa elimu huyo amesema kuwa mahudhurio ya wanafunzi waliomaliza  elimu ya msingi mwaka 2014 yameongezeka kwa 0.18%. Amesema kuwa mwaka 2013 mahudhurio siku za mitihani yalikuwa 99.02% hadi kufikia 99.2% mwaka 2014. 

Mwl. Mnyikambi ameelezea utaratibu wa kutangaza matokeo ya mtihani wa kumaliza  elimu ya msingi mwaka 2014 yanatangazwa baada ya kutangazwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ngazi ya kitaifa.  
 =30=



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...