Jumapili, 22 Februari 2015

KIHESA SEKONDARI WATAKIWA KUONGEZA UFAULU KIDATO CHA KWANZA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Shule ya sekondari Kihesa imetakiwa kujipanga vizuri kuhakikisha wanafunzi wanafaulu zaidi katika mtihani wa kumaliza kidato cha nne mwaka 2015.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alipokuwa akiongea na uongozi wa shule ya sekondari Kihesa na wananchi waliohudhuria tukio hilo la ukazugi wa ujenzi wa Maabara.
Waziri Mkuu ameitaka shule ya sekondari Kihesa yenye mikondo minne ya kidato cha nne iliwa na jumla ya wanafunzi 170 kuhakikisha angalau mikondo miwili wanapata daraja la kwanza katika mtihani wa kumaliza kidato cha nne mwaka huu 2015.
Kauli hiyo imetokana na waziri Mkuu kutoridhishwa kiwango cha ufauli wa shule hiyo kwa matokeo ya kidato cha nne kwa miaka mitatu mfululizo. Kwa mwaka 2012 na 2013 hapakuwa na daraja la kwanza wakati daraja pili walikuwa wawili (2012) na sita (2013) wakati daraja la tatu walikuwa saba (2012) na 24 (2013). Kwa mwaka 2014 daraja la kwanza alikuwa mmoja, la pili 12 na la tatu 20. Amesema kuwa matokeo hayo hayaridhishi kwa shule iliyo katika manispaa ya Iringa. Amesema kuwa shule hizo zina miundombinu imara na mazingira bora ya kusomea na kujifunzia.
Katika taarifa ya ujenzi wa Maabara katika shule ya sekondari ya Kihesa iliyosomwa kwa Waziri Mkuu na Mkuu wa shule ya sekondari Kihesa, Bwana Hudson Luhwago amesema kuwa ujenzi wa vyumba vya Maabara tatu, maboma yamekamilika na hatua inayoendelea ni ukamilishaji wa miundombinu ya ndani. Akiongelea gharama amesema kuwa hadi kukamilika kwake ujenzi huo unatarajia kugharimu shilingi 170,195,920. Amesema kuwa gharama hizo zinatokana na wastani wa shilingi 56,731,973 kwa Maabara moja. Amesema kuwa gharama hizo zimepungua kutokana na kutumia nguvu za wananchi na wadau mbalimbali.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...