Ijumaa, 20 Machi 2015

KUBORESHA MAISHA NI JUKUMU LA WADAU WOTE



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Kazi ya kuboresha maisha ya watanzania ni jukumu la wadau wote wa maendeleo wa ndani na nje ya nchi.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza katika hotuba yake iliyosomwa na Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Iringa, Bw. John Kiteve katika sherehe za uzinduzi wa Mnara mpya wa Tigi uliopo kijiji cha Magubike, Wilayani Iringa.

Mhe. Masenza amesema “kazi ya kuboresha maisha ya watanzania si jukumu la serikali peke yake bali ni la wadau wote wa maendeleo wakiwemo kampuni za simu nchini jama wanavyofanya wenzetu wa Tigo”.  Amesema kuwa kwa sababu hiyo kupitia mpango wa universal communications services access fund (UCSAF) serikali imekuwa ikishirikiana na kampuni za simu jupanua upatikanaji wa huduma za mawasiliano nchini hadi vijijini. Amesema kuwa mnara uliozinduliwa katika kijiji cha Magubike ni miongoni mwa minara inayojengwa kwa pamoja kati ya serikali na kampuni za simu katika sehemu mbalimbali nchini.

Mkuu wa mkoa waliwahakikishia wawekezaji katika sekta ya mawasiliano kuwa serikali itaendelea kushirikiana nao pamoja na wadau wengine wa maendeleo kwa kuweka mazingira bora ya utendaji kazi kwa madhumuni ya kuboresha sekta ya mawasiliano nchini. Amesema kuwa serikali inatambua kuwa uwekezaji katika huduma za mawasiliano utaleta maendeleo ya haraka katika sekta nyingine za uzalishaji kama kilimo, utalii, uchimbaji madini na biashara kwa maendeleo ya taifa.

Kutokana na huduma za mawasiliano ya simu kwa kiasi kikubwa kuwa maeneo ya mjini, Mhe. Masenza ameelezea faraja aliyopata kwa juhudi za kampuni ya Tigo kuendelea kufikisha huduma za mawasiliano ya simu vijijini. “Naipongeza sana kampuni ya Tigo kwa juhudi hizi na kuiomba iendelee kutekeleza mpango huu mzuri kwa taifa letu” alisisitiza Mhe. Masenza.

Amesema kuwa kwa mkakati huo wa kufikisha huduma za mawasiliano ya simu vijijini, Tigo inaendelea kuwa mdau muhimu katika kuchangia uboreshaji maisha ya wananchi wa Tanzania ikiwa ni sehemu ya kufanikisha utekelezaji wa Mpango wa Kupunguza Umasikini na Kukuza Uchumi Tanzania na Mpango wa Maendeleo ya Milenia.  
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...