Ijumaa, 20 Machi 2015

MAAFISA RASILIMALI WATU WATAKIWA KUTOA ELIMU YA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Maafisa rasilimali watu watakiwa kuwaelimisha waajiriwa wapya juu ya sheria inayowapa uhuru wa kuchagua mfuko wa hifadhi wanaoupenda.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza katika hotuba yake ya ufunguzi wa semina iliyosomwa na Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Iringa, Bw. John Kiteve kwa maafisa rasilimali watu waliopo mkoani Iringa iliyofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Gentle Hills Manispaa ya Iringa. 

Mhe. Masenza amesema kuwa ipo sheria inayotoa nafasi kwa waajiriwa wapya kufanya chagua la mfuko wa hifadhi ya jamii wanaoupenda na kuchangia katika kipindi cha ajira zao. Amesema kuwa sheria hiyo hairuhusu kwa mwajiriwa kuhama mfuko baada ya kuuchagua. “Hivyo ninyi kama waajiri na walezi wao mnayo dhamana ya kuwashauri juu ya ukweli huu ili wafahamu wanapoenda kufanya chaguo” alisisitiza Mhe. Masenza.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa aliapongeza GEPF kwa kuandaa semina hiyo na kuwataka kufanya semina hizo mara kwa mara ili kuweza kwenda sambamba na mabadiliko yanayoendelea kwa kasi katika sekta ya hifadhi ya Jamii nchini. Amewakumbusha kuwa elimu haina mwisho na kuwataka kuwafahamisha wadau kila linapotokea jambo jipya ili wato wafahamu na kwenda kapoja katika kulifanikisha.

Mkuu wa mkoa amepongeza juhudi za GEPF kuwakopesha wananchama wake. Amesema “mfuko wa GEPF umekuwa ukiwakopesha wanachama wake kwa kipindi kirefu sana, kupitia mikopo hii mwanachama anaweza kuchukua mpaka 45% ya mafao yake jambo ambalo ni msaada mkubwa kwa wanachama”.

Mkuu wa mkoa ameutaka mfuko wa hifadhi wa GEPF kutoa huduma bora kwa wateja. Amewataka kuutekeleza mkataba wa huduma kwa mteja kwa vitendo ili ulete maana. Aidha, amewataka kuimarisha mfumo wa utoaji taarifa kwa wanachama na matumizi ya Tehama.
=30= 








Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...