Jumamosi, 14 Machi 2015

WALIMU WATAKIWA KUWAUNGA MKONO WANAFUNZI WASOME MASOMO YA SAYANSI

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Walimu nchini wametakiwa kuachana na tabia za kuwakatisha tamaa watoto wa kike kujikita katika masomo ya sayansi kwa kisingizio kuwa ni magumu.
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Kampuni ya Rodhance, Upendo Kilale alipokuwa akiongea na mwandishi wetu katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani iliyofanyika katika uwanja wa mashujaa mjini Mafinga.
Bi. Kilale amesema kuwa wapo wasichana wengi wanaopenda kusoma masomo ya sayansi na kuonesha nia lakini wamekuwa wakikatishwa tamaa na baadhi ya walimu wao kuwa masomo hayo ni magumu. Amesema kuwa walimu wanalo jukumu kubwa la kuwatia moyo wasichana ili wasichana wengi wajikite katika masomo ya sayansi. Aidha, ameitaka jamii kwa ujumla kubadili mtazamo hasi kwa wasichana linapokuwa suala la masomo ya sayansi nchini.
Bi. Kilale amesema kuwa mwanamke aliyesoma masomo ya sayansi familia yake inakuwa na afya njema na hali bora ya kimaisha. Akiongelea zaidi suala la kiafya, amesema kuwa mwanamke aliyesoma sayansi anakuwa na uelewa mkubwa wa kuandaa chakula kwa kuzingatia uwiano wa makundi tofauti ya vyakula. Ameyataja makundi hayo kuwa ni protini, wanga, mafuta na vitamin. Amesema kuwa taifa katika kipindi hiki linakabiliwa na tatizo la lishe kutokana na jamii kushindwa kufanya uwiano wa makundi ya vyakula katika kuandaa mlo. Amesema kuwa ili kukabiliana na tatizo la lishe ni lazima wasichana ambao ni wanawake watarajiwa waandaliwa sasa kwa kuwahamasisha kusoma masomo ya sayansi.
Amesema kuwa kampuni yake inalenga kuifahamisha jamii kuwa wanawake wanaweza kufanya mambo mazuri katika masomo ya sayansi na kuitumia sayansi katika kubadilisha maisha ya kila siku.
Kampuni ya Rodhance inamakao yake makuu jijini Dar es Salaam ikiwa na tawi katika mji wa Mafinga mkoani Iringa.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...