Ijumaa, 1 Julai 2016

HALMASHAURI YA WILAYA IRINGA YAJIVUNIA NGUVUKAZI YA VIJANA KIMAERNDELEO



Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Halmashauri ya Wilaya ya Iringa inajivunia nguvukazi ya vijana katika kujiletea maendeleo na maendeleo ya Halmashauri hiyo kwa ujumla.

Akifafanua nafasi ya nguvukazi ya vijana katika Halmashauri, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Pudenciana Kisaka wakati wa mbio za Mwenge wa uhuru katika Halmashauri yake, alisema kuwa jumla ya vijana 1,321 wametumika na kupata ajira katika miradi ya kijamii. 

Aliongeza kuwa vijana wengine 1,230 walipata ajira kupitia makampuni yaliyopata zabuni za Halmashauri. Katika miradi ya barabara ni vijana 1,200 (me 900 na ke 300), na miradi ya ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji vijana ni vijana 30 (me 24 na ke 6). Alisema kuwa vijana 28,783 (me 11,781 na ke 16,877) wamewezeshwa kujiajiri na kuajiriwa. Katika sekta ya kilimo vijana 26,730, shughuli za ujasiliamali 1,372 na bodaboda 250.

Kisaka alisema kuwa ekari 198 zimetengwa katika vijiji 10 vya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kwa ajili ya vijana kuanzisha shughuli za uzalishaji mali. Katika kuimarisha na kuhakikisha upatikanaji wa mitaji, SACCOS tatu za vijana za Iringa Vijana Saccos, Mangalali na Nduli zimeundwa kwa lengo la kusaidia na kuwawezesha vijana kupata mikopo yenye masharti nafuu.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...