Ijumaa, 1 Julai 2016

TAKUKURU: JAMII TOENI TAARIFA ZA RUSHWA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Jamii imetakiwa kuwa mstari wa mbele katika kupinga vitendo vya rushwa kwa kutoa taarifa na ushirikiano kwa Takukuru ili kukabiliana na vitendo hivyo.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa dawati la uelimishaji mkoa wa Iringa, Anneth Mwakatobe alipokuwa akielezea nafasi ya jamii katika kupambana na rushwa kwenye maonesho ya shughuli za kuzuia na kupambana na rushwa katika uwanja wa mkesha wa mwenge wa uhuru katika mji mdogo wa Ifunda wilyani Iringa.

Mwakatobe alisema kuwa rushwa ni matumizi mabaya ya mamlaka anayopewa mtumishi wa umma au binafsi kwa lengo la kujinufaisha mwenyewe hivyo ni jukumu la jamii nzima kupambana na vitendo hivyo.

Akiongelea madhara ya jamii kuogopa au kukataa kushirikiana na Takukuru kufichua au kutoa ushahidi dhidi ya vitendo vya rushwa, alisema kuwa ni kuongezeka kwa vitendo vya rushwa katika jamii ambapo waathirika wakubwa wa vitendo hivyo ni jamii yenyewe. Madhara mengine ni mapambano ya rushwa kuwa magumu kwa Takukuru kuachiwa yenyewe kupambana na rushwa na kuwapa nafasi watuhumiwa wa vitendo vya rushwa kuendelea kujinufaisha.

Mwakatobe alisema kuwa Sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaaka 2007 iliongeza wigo wa kutosha kwa kuongeza makosa ya rushwa na kuipa takukuru meno zaidi. Alisema kuwa kifungu cha 15 kosa la kupokea rushwa, kushawishi kupewa rushwa, kutoa rushwa au kuahidi kutoa rushwa adhabu ni faini isiyopungua shilingi 500,000 na isiyozidi 1,000,000. Aliongeza kuwa kufungo kisichopungua miaka mitatu na kisichozidi miaka mitano au faini na kifungo kwa pamoja.

Alisema kuwa Takukuru imejidhatiti kuijengea jamii tabia ya kukataa vitendo vya rushwa kuanzia shule za msingi, sekondari na vyuo kwa kuanzisha klabu za wapinga rushwa katika maeneo hayo.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...