Jumatatu, 7 Agosti 2017

HALMASHAURI NJK ZATAKIWA KUTENGA MAENEO YA WAJASIRIAMALI



Na. Dennis Gondwe, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa

Halmashauri za mikoa ya nyanda za juu kusini zimetakiwa kutenga maeneo maalum kwa ajili ya wajasiriamali kutekeleza majukumu yao.

Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu alipotembelea mabanda ya maonesho ya Halmashuri ya Mji Makambako na Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo katika uwanja wa Nanenane mjini Mbeya.

Ayubu alisema kuwa wasindikaji katika Halmashauri wasiachwe kufanya kazi za kusindika bidhaa majumbani. 

Wasindikaji wameshuhudia kuwa wanafanya kazi za usindikaji nyumbani badala ya kufanya kazi hizo katika maeneo rasmi. Serikali likwisha zielekeza mamlaka za serikali za mitaa kutenga maeneo kwa ajili ya wajasiriamali kuweza kutekeleza majukumu yao. Maeneo hayo lazima yawe yenye miundombinu ya maji na umeme na kufikika kwa urahisi” alisisitiza Ayubu. 

Aidha, aliongeza kuwa Halmashauri ziwasaidie wajasiriamali kufikia viwango vya ubora unaotakiwa na kuwasaidia kupata nembo ya ubora ya TBS na ‘Bar cord’ ili kuweza kupata soko la ndani na nje ya nchi.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...