Jumatatu, 7 Agosti 2017

VIWANDA VIDOGO KUKUZA UCHUMI WA VIWANDA NJK



Na. Dennis Gondwe, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa

Serikali imesisitiza kuwa uchumi wa viwanda nchini unategemea sana viwanda vidogo vidogo vilivyopo katika mikoa ya nyanda za juu kusini.

Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu alipotembelea mabanda ya maonesho ya Nanenane mjini Mbeya jana.

Ayubu alisema kuwa uchumi wa viwanda unategea sana viwanda vidogo vidogo ambavyo msingi wake ni wajasiriamali wadogo. Alisema kuwa uzalishaji wa bidhaa za wajasiriamali wadogo una mchango mkubwa kwa nchi inapoelekea katika uchumi wa kati. 

“Wajasiriamali msikate tamaa, fanyeni kazi kwa juhudi zaidi, serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk John Magufuli ipo nyuma yenu kuhakikisha inawatengenezea mazingira mazuri ya kufanyia kazi” alisisitiza Ayubu. 

Aliongeza kuwa watanzania wapo tayari kununua bidhaa za ndani kwa lengo la kukuza uchumi wa wajasiriamali na taifa kwa ujumla. Changamoto iliyobaki ni kuhakikisha bidhaa zinakuwa na ubora unaokubalika kwa kuhakikisha zinakuwa na nembo ya ubora ya TBS na ‘Bar cord’.    
=30=  

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...