Jumatano, 13 Septemba 2017

KAMATI ZA KUFANIKISHA UTALII KARIBU KUSINI ZAUNDWA



Na Mwandishi Maalum, IRINGA
Kamati ya maandalizi ya Utalii mkoa wa Iringa imeunda kamati ndogo za ufuatiliaji na usimamizi wa kufanikisha maadhimisho ya siku ya Utalii Karibu Kusini na maonesho ya shughuli za viwanda vidogo kanda ya nyanda za juu kusini.

Kauli hiyo ilitolewa na mwenyekiti wa kamati ya maandalizi, Fikira Kisimba alipokuwa akiwasilisha taarifa ya maandalizi ya maadhimisho ya siku ya Utalii Karibu Kusini na maonesho ya shughuli za viwanda vidogo kanda ya nyanda za juu kunisi katika ukumbi wa Veta mjini Iringa.

Kisimba alisema kuwa katika kufanikisha maonesho hayo, kamati ya maandalizi imefanya shughuli mbalimbali pamoja na kuunda kamati ndogondogo. Kamati zilizoundwa alizitaja kuwa ni kamati ya Mipango na Fedha; Kamati ya Mapokezi, Usafiri na Malazi; Kamati ya Chakula, Afya na usafi wa Mazingira. Nyingine ni Kamati ya Miundombinu na Mapambo; Kamati ya Ulinzi na Usalama; Habari na Uenezi na Kongamano na Maonesho ya nje. 

Kisimba aliongeza kuwa kamati hizo saba zimeundwa kwa kushirikisha sekta binafsi na sekta ya umma ili kutoa uwiano sawia.

Akiongelea uhamasishaji wa jamii na mialiko, mwenyekiti huyo wa maandalizi alisema kuwa uhamasishaji unaendelea kufanyika kwa wadau mbalimbali. Alisema kuwa ofisi za SIDO katika mikoa ya nyanda za juu kusini imekwisha wataarifu wajasiriamali waliopo katika mikoa yao. Wadau wakubwa 51 wameandikiwa barua za kuomba michango na ushiriki. “Taarifa ya mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa wakati wa Maonesho ya Nane Nane - Mbeya kwa kushirikiana na Wakuu wa Wilaya na Katibu Tawala Mkoa; Vikao mbalimbali vya Maandalizi na vikao vingine vya wadau vinavyofanyika  na kushirikisha vyombo vya Habari” alisema Kisimba.
Maonesho ya Utalii yatafanyika pamoja na Maonesho shughuli za Viwanda Vidogo (SIDO) kanda ya nyanda za juu kusini kwa Mwaka 2017.  Maonesho haya yamepangwa kufanyika kuanzia tarehe 29/09/2017 hadi tarehe 02/10/2017.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...