Jumatano, 13 Septemba 2017

VYAMA VYA USHIRIKA NJK VYATAKIWA KUSHIKAMANA KUKUZA MTAJI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa
Vyama vya ushirika katika mikoa ya nyanda za juu kusini vimetakiwa kushikamana katika kukuza ushirikiano na mtaji.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, mheshimiwa Amina Masenza alipotembelea banda la Manispaa ya Iringa katika maonesho ya Nanenane katika uwanja wa John Mwakangale mjini Mbeya.

Mheshimiwa Masenza alisema kuwa wanaushirika wanatakiwa kushikamana ili kuimarisha umoja na kukuza mtaji wao. “Wanaushirika mnapopotezana, ushirika unaparaganyika. Wanaushirika tushikaname ili kudumisha ushirika hasa kina mama” alisema mheshimiwa Masenza.

Mheshimiwa Masenza alisema kuwa vijana wamekuwa wagumu kujiunga na vyama vya ushirika na kuwaacha watu wazima na wazee katika sekta ya ushirika. Aliwataka wanaushirika kubuni mbinu za kuwavutia vijana ili wajiunge na ushirika.

Wakati huohuo, mkuu wa mkoa aliwasisitiza wakina mama kuonesha ushupavu katika ushirika kusimamia na kuimarisha ushirika. Aliwashauri wakina mama kuanzisha tawi B katika ushirika kwa ajili ya watoto wao ili kuwarithisha dhana ya ushirika.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...