Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa
Chama
cha mapinduzi wilayani Mufindi kinaridhishwa na kazi zinazofanywa na serikali
ya awamu ya tano katika utekelezaji wa ilani yake na kuwahudumia wananchi.
Kauli
hiyo ilitolewa na mwenyekiti wa chama cha mapinduzi Wilaya ya Mufindi, Daud
Yassin katika ziara ya mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipotembelea
shule ya msingi Igombavanu kukagua miundombinu ya shule hiyo na kuongea na
wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya masikini TASAF wilayani humo.
Yassin
alisema “CCM wilayani Mufindi
tunafarijika na kazi zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi
wa Rais Dr. John Magufuli na wasaidizi wake. Aidha, tunaridhika na ushirikiano
tunaoupata kutoka kwa mkuu wa Mkoa wa Iringa na mkuu wa Wilaya ya Mufindi
katika kusimamia utekelezaji wa Ilani yetu”.
Alisema kuwa kazi ya chama cha
mapinduzi ni kuisimamia serikali ili itekeleze Ilani na maendeleo kwa wananchi.
Aliongeza kuwa lengo la kuisimamia serikali kutekeleza Ilani ni kuhakikisha
maisha ya wananchi wilayani Mufindi yanabadilika na kuwa bora zaidi.
Mwenyekiti
huyo aliipongeza serikali kwa uanzishaji wa mpango wa kunusuru kaya masikini
nchini. Alisema kuwa mpango huo umesaidia kurudisha matumaini kwa wananchi
wasio na uwezo na kuwawezesha kujikimu kimaisha. “Hizi ni juhudi za makusudi zinazofanywa na serikali kuonesha jinsi
inavyojali maisha ya wananchi wake” alisema.
Akiongea
na wamufaika wa mpango wa kunusuru kaya masikini katika kijiji cha Igombavanu
mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alisema kuwa serikali inawajali wananchi
wake na kutaka wawe na uhakika wa kula milo mitatu kwa siku.
“Mfuko wa TASAF umewakomboa wananchi wengi
kutoka katika maisha duni. Na huu ndiyo upendo thabiti wa serikali kwa wananchi
wake” alisema Masenza. Kupitia TASAF familia zimenufaika na watoto
wanaohudhuria shule wamenufaika kwa elimu na afya aliongeza.
Mfuko
wa maendeleo ya jamii TASAF unatekeleza mpango wa kunusuru kaya masikini katika
Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi kwa vijiji 75 vikiwa na wanufaika 6,279.
=30=
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni