Na.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa
Kamati ya kitaifa ya ushauri wa misitu imetakiwa kukamilisha rasimu ya sera mpya ya Taifa ya misitu mapema na kumshauri waziri mwenye dhamana juu ya uendelevu wa rasilimali misitu nchini.
Kamati ya kitaifa ya ushauri wa misitu imetakiwa kukamilisha rasimu ya sera mpya ya Taifa ya misitu mapema na kumshauri waziri mwenye dhamana juu ya uendelevu wa rasilimali misitu nchini.
Agizo
hilo lilitolewa na waziri wa maliasili na utalii Dr. Hamis Kigwangala alipokuwa
akifungua kikao cha tatu cha kamati ya kitaifa ya ushauri wa misitu
kilichofanyika katika ukumbi wa VETA mjini Iringa jana.
Dr.
Kigwangala alisema kuwa kamati hiyo inawajibu wa kupitia rasimu na kushauri
ipasavyo juu ya uendelevu wa rasilimali misitu.
“Hata hivyo, lipo jukumu jingine muhimu sana ambalo bila hilo utendaji
wetu katika sekta hii utakuwa mgumu sana. Jukumu hilo ni ukamilishwaji wa
rasimu ya sera mpya ya Taifa ya misitu. Kamati hii inao wajibu wa kuipitia
rasimu hii na kumshauri waziri kama inakidhi matarajio ya uhifadhi na matumizi
endelevu ya rasilimali hii au la. Hivyo, nimeridhia rasimu hii mpya kuletwa
kwenu baada ya kukamilisha hatua za kukusanya maoni toka kwa wadau tofauti
tofauti nchi nzima” alisema Dr. Kigwangala.
Aidha, aliitaka kamati hiyo
kutotumia muda mrefu kupitia rasimu hiyo na kutoa maoni yao. Alisema kuwa sera
hiyo imechelewa sana na kuitaka kamati hiyo kulipa kipaombele suala la upitiaji
wa sera hiyo.
Katika
salamu za mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alisema kuwa wizara imekuwa
ikiunga mkono juhudi za kuendeleza utalii kwa Mkoa wa Iringa na mikoa ya nyanda
za juu kusini. “Pongezi kwa juhudi za
wizara ya maliasili na utalii kuunga mkono juhudi za kuendeleza utalii mkoani
Iringa” alisema Masenza.
Aidha, alimhakikishia waziri wa maliasili na
utalii kuwa Mkoa wa Iringa umejipata vizuri katika kukuza na kuendeleza utalii
kwa ukanda wa kusini.
=30=
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni