Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Tanzania
inakabiliwa na changamoto ya uhifadhi wa misitu baada ya maeneo mengi kutokuwa
na mipaka inayotambulika rasmi.
Kauli
hiyo ilitolewa na waziri wa maliasili na utalii, Dr. Hamis Kigwangala alipokuwa
akiongea na kamati ya kitaifa ya ushauri wa misitu katika ukumbi wa chuo cha
VETA mjini Iringa jana.
Dr.
Kigwangala alisema “kwa muda huu mfupi
ambao nimekuwepo hapa katika wizara hii, nimegundua kuwa suala la uhifadhi wa
misitu ni jambo lenye changamoto nyingi sana. Na changamoto hizi hasa
zinatokana na sisi wenye dhamana ya uhifadhi wa misitu hii kwa maana ya
watendaji wa taasisi zetu, na hivyo kutoa mwanya kwa misitu yetu mingi kuvamiwa
na wananchi” alisema Dr. Kigwangala.
Alisema
kuwa wizara yake inaendelea kutekeleza maagizo ya waziri mkuu ya kuweka alama
katika misitu yote ili wananchi wapate kuitambua na kuiheshimu.
Vilevile, alikemea
tabia ya baadhi ya wananchi kugomea zoezi hilo na maeneo mengine kubomoa alama
hizo baada ya kuwekwa na wataalamu. Aliwataka wananchi kuheshimu alama hizo
ambao ni mkakati wa serikali kumaliza migogoro ya wananchi kuvamia maeneo
yaliyohifadhiwa iliyodumu kwa muda mrefu.
Katika
salamu za mkuu waa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alisema kuwa wizara imekuwa
ikiunga mkono juhudi za kuendeleza utalii kwa Mkoa wa Iringa na mikoa ya nyanda
za juu kusini.
Mkuu
wa Mkoa alisema kuwa katika kuhakikisha kuwa utalii unakuwa endelevu, Mkoa wa Iringa
umefanya utalii kuwa agenda ya kudumu katika vikao vyake. Alisema kuwa Mkoa
umejipanga kuendeleza eneo la Kihesa kilolo kwa kukuza utalii kwa kulitunza,
kuliendeleza na kulihifadhi. Utunzaji wa eneo hilo utachangia uendelevu wa sekta
ya utalii na uhifadhi mkoani Iringa na ukanda wa nyanda za juu kusini, alisema
mkuu wa Mkoa.
=30=
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni