Jumatatu, 5 Februari 2018

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAPONGEZWA KUENDELEZA UTALII IRINGA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa
Wizara ya maliasili na utalii imepongezwa kwa kuunga mkono juhudi za kuendeleza utalii Mkoa wa Iringa.

Pongezi hizo zilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipotoa salamu za Mkoa katika kikao cha tatu cha kamati ya kitaifa ya ushauri wa misitu kilichofanyika katika ukumbi wa chuo cha VETA mjini Iringa jana.
 
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza
Masenza alisema kuwa wizara imekuwa ikiunga mkono juhudi za kuendeleza utalii kwa Mkoa wa Iringa na mikoa ya nyanda za juu kusini. “Pongezi kwa juhudi za wizara ya maliasili na utalii kuunga mkono juhudi za kuendeleza utalii mkoani Iringa” alisema Masenza. 

Aidha, alimhakikishia waziri wa maliasili na utalii kuwa Mkoa wa Iringa umejipata vizuri katika kukuza na kuendeleza utalii kwa ukanda wa kusini.

Mkuu wa Mkoa alisema kuwa katika kuhakikisha kuwa utalii unakuwa endelevu, Mkoa wa Iringa umefanya utalii kuwa agenda ya kudumu katika vikao vyake. Alisema kuwa Mkoa umejipanga kuendeleza eneo la Kihesa kilolo kwa kukuza utalii kwa kulitunza, kuliendeleza na kulihifadhi. Utunzaji wa eneo hilo utachangia uendelevu wa sekta ya utalii na uhifadhi mkoani Iringa na ukanda wa nyanda za juu kusini, alisema mkuu wa Mkoa.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...