Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa
Kamati
ya kitaifa ya ushauri wa misitu imetakiwa kuangalia upya takwimu zinazoonesha mchanago
mdogo wa sekta ya misiku katika pato la taifa na kumshauri waziri mwenye
dhamana juu ya mchango wa sekta ya misitu kuongeza mchango wake.
Kauli
hiyo ilitolewa na waziri wa maliasili na utalii, Dr. Hamis Kigwangala alipokuwa
akifungua kikao cha tatu cha kamati ya kitaifa ya ushauri wa misitu kilichofanyika
katika ukumbi wa chuo cha VETA mjini Iringa jana.
Dr.
Kigwangala alisema kuwa takwimu zinaonesha kuwa sekta ya misitu inachangia
takribani asilimia 3.7 katika pato la taifa. “Sisi kama wizara haturiziki
kabisa na mchango huu. Bado tunaona uko chini sana kiasi cha kutishia
kutoaminika kwa takwimu hizo kabisa. Hili tunaona ni eneo ambalo linatakiwa kufanyiwa
kazi haraka” alisema Dr. Kigwangala.
Aidha, aliitaka kamati hiyo kuja na
ushauri wa jinsi ya kuitumia sekta ya misitu katika kuongeza mchango wake
katika pato la taifa.
Katika
salamu za mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alisema kuwa katika kuhakikisha
kuwa utalii unakuwa endelevu, Mkoa wa Iringa umefanya utalii kuwa agenda ya
kudumu katika vikao vyake.
Alisema kuwa Mkoa umejipanga kuendeleza eneo la Kihesa
kilolo kwa kukuza utalii kwa kulitunza, kuliendeleza na kulihifadhi. Utunzaji
wa eneo hilo utachangia uendelevu wa sekta ya utalii na uhifadhi mkoani Iringa
na ukanda wa nyanda za juu kusini, alisema mkuu wa Mkoa.
=30=
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni