Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Wakulima wa
halmashauri ya wilaya ya Iringa wametakiwa kulima zao la mtama na kulifanya zao
la chakula ili kukabiliana na upungufu wa chakula unaoikabili halmashauri hiyo
kutokana na hali ya ukame wa mara kwa mara.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma (katikati)
Kauli hiyo
imetolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma alipokuwa
akiongea na viongozi na wananchi wa kata za Itunundu na Pawaga katika shule ya
sekondari William Lukuvi iliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Iringa.
Mkuu wa mkoa wa
Iringa amesema kuwa kutokana na ukame wa mara kwa mara unaosababishwa na
mabadiliko ya tabia nchi, umefika wakati kwa wananchi wa kata za Itunundu na
Pawaga kulima zao la mtama. Amesema kuwa suala si kulima tu zao la mtama, bali
pia kulifanya zao hilo kuwa zao la chakula. Amesema kufanya hivyo kutawawezesha
wananchi kuwa na uhakika wa chakula kwa mwaka mzima na kuepuka tatizo la njaa.
Mkuu wa mkoa wa
Iringa amewataka wananchi mkoani Iringa kuhakikisha wanapanda miti ya kutosha
ili kukabiliana na changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi yanayosababisha ukame
katika baadhi ya maeneo ya mkoa wa Iringa.
Amesema kuwa upandaji miti huo uende
sambamba na upandaji wa miti ya matunda. Aidha, ameshauri kuwa ni vema taasisi
mbalimbali zikajikita katika upandaji wa miti ya matunda kama mapapai, maembe
na maparachichi.
Katika kuonesha
umuhimu wa upandaji miti, mkuu wa mkoa wa Iringa alishiri katika upandaji wa
mti pamoja na viongozi alioambata nao katika ziara hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa akipanda mti
=30=
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni