Jumatano, 25 Juni 2014

MLIMA KITONGA UTUNZWE VIZURI



WANANCHI wa maeneo yanayozunguka mlima Kitonga, uliopo katika wilaya ya Kilolo, mkoani Iringa wametakiwa kuutunza msitu huo kutochoma moto hovyo wala kukata miti yake, ili kuepuka athari za kimazingira zilizoanza kujitokeza duniani.
Wito huo umetolewa na afisa mipango wa wilaya ya Kilolo, Angelina Maridadi wakati akisoma taarifa ya mradi wa kuhifadhi msiti wa Kitonga baada ya Mwenge wa uhuru, kuzindua mradi huo.
Maridadi alisema wilaya ya kilolo ni miongoni mwa wilaya zinazoathiriwa kwa kiasi kikubwa na uharibifu wa mazingira jambo ambalo, lazima lipigiwe kelele ili jamii iachane nalo.
“Wananchi wa kilolo tusaidiane kuhifadhi mazi”
Alisema kuwa kuanzishwa kwa mradi huo kumetokana na mkakati wa wilaya hiyo katika kuendelea kuhifadhi misitu ya asili, kwa kusimamia sheria za kudhibiri uharibifu wa mazingira na kuhamasha jamii kujali maeneo hayo.
Alisema, eneo la msitu wa hifadhi Kitonga linamiti mingi ya asili aina ya miyombo na kwamba, mradi huo unavihusisha vijiji vya vitatu vinavyozunguka eneo hilo.
Maridadi alisema mpaka sasa tayari zimeanza kutumika sh milioni 59 kwa ajili ya kuendeleza msitu huo, na kwamba wananchi wa maeneo husika ndio wasimamizi wakuu wa maeneo hayo.
Akizindua mradi huo, Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa, Rahel Kassanda aliisisitiza jamii kuendelea kulinda misitu hiyo kwa kutoharibu mazingira ikiwemo tabia za kuchoma moto na kukata miti hovyo.
Alisema misitu ikihifadhiwa itasaidia kulinda vyanzo vya maji ambavyo vitaongeza uzalishaji wa chakula katika maeneo hayo na kusaidia kuinua uchumi wa nchi.
Kassanda alisema mkoa wa Iringa kwa miaka mingi umekuwa ukisifika kwa hatua za utunzaji wa mazingira na kwamba, ikiwa misitu itaendelea kutunza unaweza kuendelea kuwa na sifa hiyo.
Mwisho.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...