Jumatano, 25 Juni 2014

WAKULIMA WA CHAIWAKABIDHIWA MATREKTA 6



Frank Kibiki- KILOLO
VIKUNDI vya wakulima wa zao la chai wilayani Kilolo, mkoani Iringa wamekabidhiwa matrekta sita yenye thamani ya sh milioni 318 ili kusaidia kufufua kilimo chazao hilo ambacho kimedorora katika wilaya hiyo.
Kukabidhiwa kwa matrekta hayo kunawaletea tumaini jipya wakulima wa wilaya ya Kilolo, ambao walianza kukata tamaa ya kulima zao hilo wakihofia soko.
Akikabidhi matrekta hayo, Kiongozi wa mbio za Mwenge, Rahel Kassanda alisema kilimo cha jembe la mkoni kimepitwa na wakati na kwamba, ili uzalishaji wa mazao wa kilimo uongezeka ni lazima kutumia zana za kisasa.
Aliwataka wakulima hao kutunza matrekta waliyokabidhiwa, ili yawasaidie katika kuendesha kilimo cha kisasa ambacho kitawawezesha kuondokana na ugumu wa maisha.
Akisoma taarifa ya wakulima hao, kaimu afisa kilimo wa wilaya ya Kilolo, Edward Mbembe alisema mradi wa matrekta ulianza mwaka 2013 ukiwa na lengo la kuendeleza mnyololo wa thamani wa zao la chai, kwa vikundi vya wakulima wadogo wa wilaya hiyo.
Alivitaja vikundi vilivyokabidhiwa matrekta hayo kuwa ni Luhindo, Masisiwe, Mwatasi, Kidabaga, Idete na Kimala.
Mbembe alisema wakulima hao waliweza kuchangia sh milioni 78 huku halmashauri ya wilaya kupitia mpango wa maendeleo ya kilimo, ilichangia sh milioni 240.
Wakizungumza na uhuru, wakulima wa zao hilo walisema matrekta hayo yatawasaidia katika kujikwamua kiuchumi kwa kuendesha kilimo cha kisasa ambacho, hawajawahi kukilima.
Aidha waliiomba serikali kujenga kiwanda cha chai wilayani humo ili iwe rahisi kwao kuuza raslimali hiyo tofauti na sasa ambapo, watagemea viwanda vya wilaya nyingine.
Mwisho.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...