Jumatano, 25 Juni 2014

WANAWAKE WAJIUNGE NA VIKUNDI KUONDOA UMASIKINI



NA FRANK KIBIKI, KILOLO
WANAWAKE wametakiwa kujiunga kwenye vikundi vya kiuchumi na kufanya kazi kwa bidii ili waweze kuondokana na ugumu wa maisha unaowakabili.
Kiongozi wa mbio za Mwenge, Rahel Kassanda alitoa wito huo jana wakati akikabidhi hundi ya sh milioni moja, kwa kikundi cha wanawake cha Tuinuliwe, kilichopo katika kijiji cha Masukanzi, wilayani Kilolo.
Kassanda alisema kikundi hicho ni mfano wa kuigwa na wanawake ambao wamekuwa wakisubiri kupatiwa fedha na waume zao badala ya wao kushiriki katika uzalishaji.
Alisema ikiwa kundi la wanawake, litataka kuondokana na ugumu wa maisha, ni lazima kuungana pamoja kwa kuanzisha vikundi ili iwe rahisi kupatiwa mikopo yenye riba naafuu na hatimaye kuondokana na umaskini.
Aliwataka wanawake wa kikundi hicho kutumia fedha za kikundi hicho kwa malengo yaliyokusudiwa mara wanapokopa ili kutoa naafasi kwa wengine kuendelea kukopesha.
Akisoma taarifa ya kikundi hicho, Katibu wa kikundi hicho Jumanne Tembo alisema wanawake waliojiunga kwenye kikundi hicho wamefanikiwa kuondokana na umaskini.
Alisema tayari serikali kupitia halmashauri ya wilaya ya Kilolo, iliwapatia mkopo wenye thamani ya sh milioni 4.4 ambazo wametumia kununulia bajaji ya mizigo, ikiwa ni mradi wa kikundi.
“Tulianza tikiwa hatuna kitu, tukaweza kuwekeza sh lakini 240, na sasa tumepata mtaji wa sh milioni 4.4 fedha ambayo kama tungebweteka nyumbani, tusingeipata,” alisema Tembo.
Mbali na masuala ya kiunchumi, wanawake hao wamekuwa wakitumia muda mwingi kujifunza masuala mbali mbali likiwemo janga la ukimwi.
Mwisho.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...