Jumatano, 4 Juni 2014

VIJANA IRINGA WASHIRIKISHWE KATIKA KILIMO



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dkt. Christine Ishengoma ameutaka uongozi wa wilaya ya Iringa kuwashirikisha vijana katika shughuli za kilimo ili waweze kujikwamua na umasikini.

Dkt. Ishengoma ameyasema hayo alipotembelea skimu ya umwagiliaji ya Kiwere-Mgera kukagua utendaji wake wa kazi katika ziara ya kukagua shughuli za maendeleo wilayani Iringa.

Mkuu wa Mkoa aliwashuhudia baadhi ya vijana wakijishughulisha na kilimo katika skimu hiyo. Amesema kuwa lengo la serikali kujenga na kuimarisha skimu hiyo ni kuwawezesha wananchi waweze kujihusisha na kilimo kikamilifu. Amesema lengo la serikali ni kuhakikisha wananchi wanafanya kilimo cha uhakika na chenye tija.   

Ameutaka uongozi wa wilaya kuwashirikisha vijana katika sekta ya kilimo ili sekta hiyo iendelee kutoa mchango katika maendeleo yao na mkoa kwa ujumla. Amesema kuwa vijana na kundi muhimu sana katika jamii na nguvu kazi katika shughuli za maendeleo ya mkoa.

Dkt. Ishengoma ameagiza kuwa wakulima katika skimu hiyo wajikite katika kilimo cha matunda mbalimbali ili kujiongezea kipato. Ameyataja baadhi ya matunda yanayoweza kulimwa hapo kuwa ni maembe, mapapati, matango.

Akiongelea manufaa yanayotokana na skimu hiyo ya umwagiliaji, Mwenyekiti wa skimu ya umwagiliaji ya kiwere-mgera Raphael Myinga amesema ametoa shukrani kwa serikali kwa ujenzi wa skimu hiyo ya umwagiliaji inayohudumia zaidi ya hekta 350 katika wilaya ya Iringa. Amesema kuwa skimu hiyo imekuwa na manufaa makubwa katika eneo hilo kwa sababu imewawezesha vijana kujishughulisha katika kilimo na kuachana na masuala mengine hasa ya kuhatarisha amani wilayani Iringa. 

Amesema kuwa kutokana na manufaa ya skimu hiyo wananchi wamenufaika na kilimo na mauzo ya mazao yatokaanayo na kilimo. Amesema kuwa vijana wameweza kununua vyombo vya usafiri kama pikipiki na magari na ujenzi wa nyumba pamoja na mambo mengine.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...