Jumapili, 10 Agosti 2014

AJARI ZA BARABARANI ZINAEPUKIKA- DKT. ISHENGOMA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa- IRINGA
Ajali za barabarani zinaweza kuepukika iwapo waendesha pikipiki watazingatia sheria na kanuni za usalama barabarani.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma alipokuwa akizindua gari la kubeba majeruhi na kufunga mafunzo ya madereva wa pikipiki Mkoani Iringa yaliyofanyika katika uwanja wa michezo wa kumbukumbu ya Samora mjini Iringa.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma (kushoto) akikata utepe kuzindua gari la wagonjwa
Dkt. Ishengoma amesema “sote tunatambua kwamba miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la ajali za barabarani zinazosababisha vifo kwa watu wengi. Ajali hizo zinahusisha pikipiki. Ajali hizo zinaweza kuepukika endapo waendesha na wapanda pikipiki watazingatia sheria na kanuni za usalama barabarani”.  Aidha, ametoa wito kwa waendesha pikipiki kuacha tabia ya kuendesha pikipiki bila kupata mafunzo na kutokuwa na leseni, kuzingatia sheria ya kuvaa kofia ngumu kwa dereva na abiria na kuacha tabia ya kubeba abiria zaidi ya mmoja katika pikipiki moja. 
Dkt. Christine Ishengoma (Mb.)
Mkuu wa Mkoa wa Iringa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinza na Usalama Mkoa wa Iringa amewataka watumiaji wengine wa barabara kuzingatia sheria za usalama barabarani. Vilevile, amewataka abiria wa mabasi na magari yote kuzingatia ufungaji wa mikanda kwa usalama wao. Wakati huohuo amekemea tabia ya abiria kushabikia mwendokasi na kukataa kujazwa kwenye mabasi zaidi ya idadi inayotakiwa.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...