Ijumaa, 1 Agosti 2014

MAZINGIRA MAZURI YA UWEKEZAJI YAVUTA MITAJI NCHINI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-IRINGA
Mazingira mazuri ya uwekezaji ni jambo lililochangia kuvutia wawekezaji mitaji nchini.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu- Uwekezaji na Uwezeshaji Dkt. Mary Nagu alipokuwa akimkaribisha Waziri Mkuu kufungua kongamano la uwekezaji kwa mikoa ya Iringa, Njombe na Mbeya lililofanyika jijini Mbeya.

Dkt. Nagu amesema kuwa mazingira mazuri ya uwekezaji nchini Tanzania yamewezesha kuvutia wawekezaji mitaji. Amesema Tanzania imevutia mitaji mingi zaidi hadi kufikia mwaka 2013 dola za kimarekani shilingi Bilioni 1.87 zaidi katika sekta ya utafutaji madini,nishati na gesi.

Akiongelea uwezeshaji wa ndani, Waziri wa Nchi OWM-UU amesema kuwa uwekezaji wa ndani ni jambo muhimu katika ukuzaji wa uchumi nchini. Amesema kuwa uwekezaji wa ndani ni muhimu kwa sababu faida kubwa inabaki ndani ya nchini. Aidha, ametoa wito kuhakikisha kila uwekezaji unamletea mwananchi mafanikio yanayoonekana na si mafanikio ya kihisia.

Waziri Dkt. Nagu amesema kuwa kongamano ni muhimu na litakisaidia kituo cha uwekezaji nchini (TIC) kuainisha fursa za uwekezaji zilizopo kwa lengo la kuvutia uwekezaji zaidi. Amesema kuwa kongamano hilo litasaidia kuandaa takwimu sahihi za miradi inayohitaji uwekezaji katika ukanda wa Nyanda za Juu Kusini. Aidha, amewashauri wawekezaji wa ndani kukitumia ipasavyo kituo cha Taifa cha uwekezaji ili waweze kunufaika na shughuli za kituo hicho. Amesema kuwa TIC ikitumika ipasavyo kutapunguza na kuepuka matapeli wanaojichomeka kwa jina la kuto hicho cha uwekezaji kwa lengo la kujinufaisha.

Dkt. Nagu ameutaja ukanda wa kusini kuwa ni ukanda wenye rasilimaji nyingi kuliko kanda zote na kuwataka wawekezaji kutumia fursa ya rasilimali hiyo kujiletea maendeleo.

Waziri Dkt. Nagu amezitaja changamoto zinazoikabili mikoa ya Iringa, Njombe na Mbeya kuwa ni usafiri hasa wa reli na barabara. Amesema kuwa serikali imeanza kukabiliana na changamoto hizo kwa kuimarisha miundombinu ya reli na barabara ili kuzifanya changamoto hizo kuwa historia.

Kongamano hili ni muendelezo wa utaratibu uliowekwa kuweza kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo na ambazo hazijavumbuliwa.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...