Ijumaa, 1 Agosti 2014

WAWEKEZAJI WAALIKWA IRINGA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa- IRINGA
Mkoa wa Iringa umewaalika wawekezaji kuwekeza katika sekta ya kilimo pamoja na sekta nyingine ili kuinua uchumi wa wananchi wake.

Mualiko huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma alipokuwa akitoa neon la ufunguzi katika kongamano la uwekezaji kwa mikoa ya Iringa, Njombe na Mbeya lililofanyika katika ukumbi wa Mkapa jijini Mbeya.

Dkt. Ishengoma amewataka wawekezaji kutumia fursa za uwekezaji katika kilimo. “Kilimo ni muhimu na muhimili mkuu ukitoa ajira kwa asilimia 85. Hali ya hewa kwa ustawi wa mazao ya chakula na biashara na ufugaji” alisisitiza Dkt. Ishengoma. Amesema kuwa msisitizo ni uwekezaji katika kilimo cha umwagiliaji. Ameyataja mazao makuu yanayolimwa Iringa kuwa ni mahindi, mpunga, maharage, ndizi, maua na matunda. Aidha, amesisitiza kuwa mazao yote yanastawi katika mkoa wa Iringa.

Mkuu wa Mkoa amekaribisha uwekezaji katika sekta za elimu na afya. Amesema kuwa pamoja na jukumu lililofanywa na serikali katika kuwekeza kwenye sekta za elimu na afya bado uwekezaji unahitajika katika maeneo ya miundombinu hasa ujenzi wa maabara na mabweni. Maeneo mengine ni ujenzi wa miundombinu ya afya na huduma za afya kwa ujumla wake. Amesema pia fursa ipo katika ujenzi wa vyuo vya uuguzi na udaktari katika mkoa wa Iringa ili kusaidia kukabiliana na upungufu wa wataalamu katika fani hizo.

Dkt. Ishengoma amesema kuwa pamoja na mkoa kujivunia mtandao mzuri na imara wa barabara kwa ajili ya kusafirisha mazao na malighafi mbalimbali, mkoa bado unahitaji wawekezaji katika viwanda vya usindikaji mazao na matunda.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...