Jumapili, 7 Septemba 2014

GHALA LA KISASA LAZINDULIWA KIDAMALI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa IRINGA
Wananchi wa Kidamali watanufaika na ghala la mbolea kwa kupata mbolea na pembejeo za kilimo na ongezeko la kipato kwa kaya.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma katika hotuba yake ya uzinguzi wa ghala la mbolea Kidamali wilayani Iringa iliyosomwa na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na sekta za Uzalishaji, Adam Swai.

Dkt. Ishengoma amesema kuwa kupitia ghalalinalozinguliwa leo wananchi wanatarajia kunufaika na uwepo wa wataalamu wa kampuni ya Yara watakaotoa ushauri kuhusu kanuni za kilimo bora katika kipindi chote cha kilimo. Manufaa mengine ameyataja kuwa uwepo wa mbolea mbalimbali za kupandia, mbolea za kukuzia na uwepo wa pembejeo nyingine za kilimo kama mbegu bora, dawa za magugu, wadudu na magonjwa kwa kipindi chote cha kilimo. Faida ndingine ni ongezeko la kipato na kuboresha maisha.

Mkuu wa Mkoa amewataka kulitumia vizuri ghala hilo kwa kiwango kinachopendekezwa na kitaalamu ili wananchi wengi waweze kuongeza uzalishaji wa mazao kwa kila ekari jambo litakaloongeza mapato. Amesema kuwa kufanya hivyo kutaongeza uhakika wa chakula katika kaya, kuongeza kipato na kupunguza umasikini.
Akiongelea mapinduzi ya kilimo, Dkt. Ishengoma amesema “ili tuweze kuleta mapinduzi ya kilimo na kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara kwa wingi kwa kila ekari inayolimwa ni lazima tulime kitaalamu. Tunatakiwa tupime na kujua hali ya rutuba katika mashamba yetu. Maeneo mengi rutuba katika udongo imepungua sana. Kuna upungufu mkubwa wa viini lishe vya Naitrojeni, Fosforasi, Potassium, Boron, Zinc na Sulfur”.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...