Jumapili, 7 Septemba 2014

HOSPITALI YA RUFAA IRINGA YAPATIWA MASHINE ZA KISASA ZA KUPIMA JOTO



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa imepatiwa mashine za kisasa za kupima joto kwa wagonjwa kwa lengo la kuboresha huduma hospitalini hapo.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Robert Salim (kulia) akimkabidhi Mashine Dkt. Issack Mlay

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Robert Salim (katikati) akimkabidhi Mashine Dkt. Tatu Mbotoi (kushoto)

Infrared Thermometer 

Kauli hiyo imetolewa na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa, Dkt. Robert Salim alipokuwa akikabidhi mashine za kupima joto (Infrared Thermometer) kwa Dkt. Tatu Mbotoni ambaye ni Daktari wa Magonjwa ya kawaida ya watu wazima mashine (2) na Dkt. Issack Mlay ambaye ni Daktari wa watoto mashine (1).

Dkt. Salim amesema kuwa lengo la kukabidhiwa mashine hizo ni kuifanya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa kuwa ya kisasa katika utoaji huduma kwa wagonjwa. Amesema kuwa mashine hizo ni nzuri kwa sababu zinauwezo wa kupima joto pasipo kugusana na mgonjwa. Amesema kuwa mashine hizo ni muhimu hasa katika kipindi hiki ambapo ugonjwa wa Ebola umeendelea kuwa tishio barani Afrika.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Iringa ameshukuru kwa msaada huo na kutoa wito kwa wadau wengine kujitokeza kuisaidia hospitali hiyo ili iweze kutoa huduma kwa wananchi. Aidha, amewataka waliokabidhiwa mashine hizo kuzitumia vizuri kwa malengo yaliyokusudiwa.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...