Jumatatu, 8 Septemba 2014

PLANTWISE KUPUNGUZA UPOTEVU WA MAZAO



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
 Mpango wa usalama wa chakula wa kimataifa unaolenga kupunguza upotevu wa mazao kutokana na magonjwana kuimarisha usalama wa chakula.

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Nuhu Mwasumilwe katika hotuba yake ya ufunguzi iliyosomwa kwa niaba yake na Afisa Kilimo Mkuu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Grace Macha wakati wa uzinduzi wa Kliniki ya Mimea kituo cha rasilimali cha Kata ya Ifunda wilayani Iringa.
Grace Macha akisoma hotuba

Huduma nayo ilitolewa papohapo

Mwasumilwe amesema kuwa Plantwise ni mpango wa usalama wa chakula wa kimataifa wenyr lengo la kuzisaidia nchi washirika kuwapatia wananchi maarifa yanayohitajika ili kupunguza upotevu wa mazao kutokana na magonjwa na kuimarisha usalama wa chakula kwa kupata usahihi wa taarifa kuhusiana na afya ya mimea. 

Amesema kuwa duniani inakadiliwa kuwa watu bilioni moja wana upungufu wa chakula kila siku na nusu ya idadi hiyo ni wakulima wadogo wadogo ambao wanategemea mazao kwa chakula na kipato kwa maisha ya kila siku.

Kaimu Katibu Tawala Mkoa amesema kuwa asilimia 40 ya mazao yanayolimwa duniani kote hupotea kutokana na magonjwa na wadudu waharibifu. Amesema kuwa kutokana na idadi kubwa ya watu duniani udhibiti na upotevu wa mazao unahitaji hatua za haraka. Amesema kuwa iwapo upotevu huo utapunguzwa kwa asilimia moja upo uwezekano wa kulisha watu wengi zaidi. Amesema kuwa katika kufanikisha hilo wakulima wanahitaji ushauri, watafiti wanahitaji kutoa taarifa sahihi na watunga sera wanahitaji zana kwa ajili ya kufanya maamuzi.

Akiongelea malengo ya Mpango huo ameyataja kuwa ni kuwasaidia wakulima wadogo wadogo kupunguza kiwango cha upotevu wa mazao kutokana na baa la magonjwa ya mimea na wadudu waharibifu. Ameongeza malengo mengine kuwa ni kutoa taarifa ya mtawanyiko wa wadudu waharibifu na magonjwa ya mimea na afya ya mimea kote duniani na kuzifanya taarifa hizo kupatikana kwa urahisi.

Mpango huu wa Plantwise ulianzishwa mwaka 2002 ukijulikana kama Kliniki ya Mimea Duniani.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...