Alhamisi, 11 Septemba 2014

MTIHANI WA DARASA LA SABA MKOANI IRINGA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa IRINGA
Maandalizi ya mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi mwaka 2014 mkoani Iringa yamekamilika na jumla ya wanafunzi 21,540 wanatarajiwa kufanya mtihani huo.
Mwl. Joseph Mnyikambi
Kauli hiyo imetolewa na Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Elimu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mwl. Joseph Mnyikambi alipokuwa akiongea na waandishi wa Habari kuhusu maandalizi ya mtihani huo utakaoanza tarehe 10-11/9/2014 kwa mkoa wa Iringa ofisini kwake.
Mwl. Mnyikambi amesema “jumla ya wanafunzi 21,540 (wavulana 9,779 na wasichana 11,761) ndiyo watafanya mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi mwaka 2014”. Amesema kuwa idadi ya wanafunzi watakaofanya mtihani huo imepungua ikilinganishwa na mwaka 2013 ambapo kulikuwa na watahiniwa 23,149 (wavulana 10,753 na wasichana 12,396) waliosajiliwa.
 Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Elimu amesema kuwa maandalizi yote yamekamilika na vifaa vyote vinavyohusiana na mtihani huo tayari vimepelekwa kwenye Halmashauri zote za Mkoa wa Iringa.
Aidha, ametoa wito kwa wazazi wenye watoto wanaosoma darasa la saba kuhakikisha watoto wao wanakwenda kufanya mtihani huo. Amewataka wanafunzi wote wa darasa la saba kuzingatia maelekezo watakayopewa na wasimamizi.
Waandishi wa Habari

Waandishi wa Habari
Mkoa wa Iringa una jumla ya shule za msingi 484 kati ya shule hizo shule 458 ndizo zenye wanafunzi watakaofanya Mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi mwaka 2014.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...