Ijumaa, 14 Novemba 2014

Matumizi bora ya Choo yanapunguza Magonjwa



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Matumizi ya choo bora na kunawa mikono kwa sabuni ni njia bora ya kupunguza magonjwa ya kuhara kwa asilimia 32.

Kauli hiyo imetolewa na mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Iringa Dkt. Leticia Warioba, katika uzinduzi wa maadhimisho ya choo duniani, siku ya kunawa mikono duniani na wiki ya usafi wa kimkoa yaliyofanyika katika kijiji cha Ifunda wilayani Iringa.
 
Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Dkt. Leticia Warioba
Dkt. Warioba amesema “matumizi ya choo bora na kitendo rahisi cha kunawa mikono kwa sabuni ni moja ya njia bora ya kuokoa maisha ya watoto na jamii nzima kwa ujumla. Kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka msalani/chooni hupunguza kuenea kwa magonjwa ya kuhara na manufaa yake ni ya muda mrefu kwa afya na ustawi wa watoto na jamii kwa ujumla”.

Amesema kuwa takwimu zinaonesha kuwa matumizi ya choo bora hupunguza magonjwa ya kuhara kwa asilimia 32 na kunawa mikono kwa sabuni hupunguza magonjwa hayo kwa asilimia 50.
Amesema kuwa shirika la afya duniani limeainisha kuwa watu wengi duniani wanapata au kumiliki huduma za simu za mkononi kuliko wanaopata huduma za choo bora. Kati ya watu bilioni 7 duniani kote, watu bilioni 6 wanamiliki au hupata huduma ya simu na watu bilioni 4.5 tu ndio wanamiliki au hupata huduma ya choo bora. Amesema kuwa tafsiri hiyo inamaanisha kuwa watu bilioni 2.5 duniani hasa maeneo ya vijijini hawana huduma ya vyoo. 
 
Afisa Afya Mkoa, Khadija Haroun

Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa, Scolastica Mlawi

Nae Afisa afya Mkoa wa Iringa, Khadija Haroun amelitaja lengo la maadhimisho hayo kuwa ni kuihamasisha jamii kuchukua hatua katika kukabiliana na changamoto za kukosa huduma za choo bora na unawaji wa mikono kwa sabuni na hatimae kumaliza kabisa tatizo la huduma hizi muhimu. Ameongeza kuwa maadhimisho hayo yanalenga kuepusha magonjwa yanayoweza kuambukizwa kupitia kukosa huduma za vyoo na unawaji wa mikono usio wa kitaalamu.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...