Alhamisi, 19 Februari 2015

SERIKALI KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA ASEMA PINDA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kuboresha huduma za afya katika hospitali na vituo vya afya ili kutoa huduma bora kwa wananchi.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda baada ya kukagua na kuzindua kituo cha Afya Mlowa kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa.
Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda

Mhe. Pinda amesema “serikali yenu inajitahidi na itaendelea kuboresha huduma za afya katika hospitali na vituo vya afya ili huhakikisha huduma bora kwa wananchi wake”. Amesema kuwa ni lengo la serikali huona wananchi wake wanakuwa na afya bora kutokana na huduma bora za afya.

Akiongelea magonjwa yanayowaathiri zaidi kina mama, Waziri Mkuu ameyataja kuwa ni saratani ya mlango wa kizazi, fistula na saratani ya matiti. Ameutaka uongozi wa wilaya ya Iringa kuwaelimisha wananchi juu ya dalili za magonjwa hayo. Amesema kuwa magonjwa hayo yanatibika pindi dalili zake zinapogundulika mapema. Amesema kuwa magonjwa haya yasipotibika mapema huweza kusababisha maambukizi mengine kwa kina mama na kufanya matibabu yake kuwa magumu zaidi na hatimae kusababisha vifo vinavyoweza kuzuilika.

Kwa upande wa magonjwa yanayowakabili wanaume kwa wingi, ameyataja kuwa ni shinikizo la damu na saratani ya tezi dume. Amesema wanaume wengi wanakabiliwa na shinikizo la damu kutokana na wingi wa majukumu waliyo nayo. 

Katika taarifa ya mradi wa ujenzi wa kituo cha afya Mlowa iliyosomwa kwa Waziri Mkuu na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Bibi Pudenciana Kisaka amesema kuwa kutokana na umuhimu wa sekta ya afya katika halmashauri ya wilaya ya Iringa, iliamua kuchangia shilingi 61,534,000. Amesema kuwa wadau wengine waliochangia ni serikali ya Japan kupitia Jica iliyochangia shilingi 111,000,000 na wadau wengine wa maendeleo hadi kufikia shilingi 197,789,000.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Bibi Pudenciana Kisaka

Kituo cha afya Mlowa kinahudumia wananchi 4,347 wa vijiji vya Malinzanga, Mafuruto na Nyamahana.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...