Jumapili, 1 Machi 2015

KILOLO WATAKIWA KUUNDA HALMASHAURI MBILI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Wilaya ya Kilolo imeshauriwa kuunda Halmashauri mbili ili kuwarahisishia na kuharakisha maendeleo ya wananchi.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda alipokagua skimu ya umwagiliaji ya Nyanzwa iliyopo Wilayani Kilolo.
Mhe. Pinda amesema “kwa kuzingatia hali halisi ya jiografia ya Wilaya ya Kilolo ambayo ina wakazi wanaoishi milimani na wengine wanaishi mabondeni, nashauri uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo na uongozi wa Mkoa ukae pamoja na kuangalia uwezekano wa kuanzisha Halmashauri mbili (2). Halmashauri moja ishughulikie maendeleo ya wananchi wanaoishi milimani na Halmashauri ya pili ishughulie maendeleo ya wananchi wanaoishi mabondeni kwa kuwa mazingira yao ni tofauti.” Amesema kuwa hatua hiyo itasogeza huduma za maendeleo karibu na wananchi tofauti na hali ilivyo sasa. Ameutaka uongozi wa Mkoa kuwasilisha mapema maombi hayo Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI.
Aidha, ameutaka uongozi wa Halmashauri ya Kilolo kutazama upya ukubwa wa maeneo ya utawala ya Kata zake na kuzigawanya kwa kuwa kwa sasa maeneo ni makubwa sana jambo ambalo linasababisha wananchi kukosa huduma za muhimu karibu.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...