Jumapili, 1 Machi 2015

MANISPAA IRINGA WATAKIWA KUHUISHA MPANGO WA MJI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Halmashauri ya Manispaa ya Iringa umetakiwa kufanya mapitio ya Mpango wa Mji kwa kushirikisha wataalam wa Chuo kikuu cha Ardhi.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda alipokuwa akiongea na wananchi wa Manispaa ya Iringa katika uwanja wa shule ya msingi Ipogolo iliyopo katika Manispaa ya Iringa.
Mhe. Pinda amesema kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ina historia ndefu kwa kuwa ilitangazwa kuwa Mji mwaka 1955 na kuwa Manispaa mwaka 1988. Manispaa ya Iringa ina Kata 18 na Mitaa 192 na Wakazi 150,000. Amesema kuwa changamoto yake kubwa ni kuwa na eneo dogo la Kilometa za Mraba 331 tu, sawa na takriban asilimia moja ya eneo la Mkoa ambalo ni Kilometa za Mraba 35,700.
”Nashauri uongozi wa Manispaa ya Iringa mfanye mapitio ya Mpango wa Mji wa Manispaa ya Iringa (Master Plan) kwa kushirikiana na Wataalam kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi ili Mji wenu upangwe vizuri zaidi na mpime viwanja kwa utalaam wa kisasa” alisema Mhe. Pinda.
Ameitaka Halmashauri hiyo kujitahidi kuwa mbele ya wananchi kwa kupima viwanja ili kuepuka wananchi kujijengea makazi yao kiholela halafu baadaye wanawabomolea nyumba zao nzuri. Amewakata lengo lao liwe kuwawezesha wananchi kujenga nyumba bora katika maeneo yaliyopimwa viwanja. Waziri Mkuu alitumia mkutano huo kuziagiza Halmashauri zote nchini ziimarishe Idara za Mipango Miji na zikope kwa ajili ya kupima viwanja.
=30=





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...