Jumapili, 1 Machi 2015

REA KUFIKIA VIJIJI 94 IRINGA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Vijiji zaidi ya 20 vimesambaziwa huduma ya umeme na REA Mkoani Iringa kufikia mwaka 2014.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza katika taarifa aliyoisoma kwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda Ikulu ya Iringa.
Mhe. Masenza amesema kuwa Wakala wa Umeme Vijijini (REA) wamefanikiwa kusambaza umeme katika vijiji mbalimbali vya Mkoa wa Iringa. Katika kipindi cha mwaka 2010-2014 jumla ya vijiji 21 vilikuwa vimepewa huduma ya umeme. Amesema kuwa kwa mwaka wa fedha 2014/2015, REA wanatarajia kuvipatia huduma ya umeme vijiji 94 katika Mkoa wa Iringa.
Akiongelea miradi ya umeme vijijini katika majumuisho ya ziara yake Mkoani Iringa, Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda ameitaka Wizara ya Nishati na Madini na Wakala wa Umeme Vijijini kuongeza kasi ya usambazaji ili vijiji vingine viweze kupata umeme mapema iwezekanavyo.
Amesema kwa mujibu wa mtandao wa Wakala wa Umeme Vijijini, vijiji vitakavyopatiwa umeme kwa Mkoa wa Iringa kwa Grid ya Taifa 2014/2015 kuwa ni vijiji vya Idodi, Tungamalenga, Hifadhi ya Taifa Ruaha, Pawaga, Ikuvilo, Isimila, Mlanda, Ng’enza, Mgama, Kiponzero, Itengwilinyi, Lupembe, Lwasenga, Kiwere, Mfihome, Muhefu na Kitapilimwa (Vijiji 17) vyote Iringa vijijini.
Vingine ni vijiji vya Ilamba, Lukani, Ihimbo, Utengule, Ibumi, Image, Mtitu, Pomerine, Bomalang’ombe, Mwatasi, Stendi ya Mbuzi, Imalutwa, Lugalo, Kitumbuka, Luganga-Kibaoni, Lusinga, Shule ya Sekondari Udzungwa, Dabaga, Irole na Maria Consolata (Vijiji 20) katika Wilaya ya Kilolo.
Vijiji vingine ni Kibengu, Usokami, Mapanda, Ukami, Ihimbo, Ilongombe, Kipanga, Igeleke, Uhafiwa, Ihalamba, Wamia, Vikula, Nundwa, Ugesa, Kidilu, Ilusa, Madibira, Idofi, Nyigo, Iramba, Mbalamaziwa, Malangali Sekondari, Ihowanza, Kwatanga, Ikongozi, Kilimanzowo, Mtambula, Udumuka, Lugolofu, Ihomasa na Kituo cha Afya Nyololo (Vijiji 32) katika Wilaya ya Mufindi.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...