Jumamosi, 29 Aprili 2017

KIKOSI KAZI KUNUSURU MTO RUAHA CHARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI AGIZO TOMMY DIARIES FARM



Na Dennis Gondwe, IRINGA
Kikosi kazi namba tatu cha kunusuru ikolojia ya mto Ruaha mkuu kimeridhishwa na utekelezaji wa agizo la kuondoa migomba isiyo rafiki kwa vyanzo vya maji katika shamba la mifugo la Tommy diaries lililopo wilayani Kilolo.

Kauli hiyo ilitolewa jana na wakili wa serikali mkuu kutoka baraza la Taifa la la hifadhi ya mazingira (NEMC), Benard Kongola baada ya kikosi kazi hicho kwenda kufuatilia utekelezaji wa agizo la tarehe 24/4/2017 lililomtaka muwekezaji huyo kuondoa migomba hiyo shambani kwake wilayani kilolo.
Mwanasheria wa NEMC Benard Kongola (kulia) akikaguautekelezaji wa agizo la ukataji migomba ndani ya kingo za mto Ruaha katika shamba la Tommy Diaries

Kongola alisema “migomba ambayo si rafiki kwa vyanzo vya maji ilikuwa imepandwa ndani ya mita 60 kutoka kingo za mto Ruaha mdogo jambo ambalo ni ukiukwaji wa sheria ya Mazingira ya mwaka 2004, sehemu ya 57 ibara ndogo ya 1 inayozuia kulima au kufanya shughuli za kibinadamu ndani ya mita 60”. 

Alisema kuwa walipotembelea shamba hilo kukagua hali ya uhifadhi wa mazingira na ikolojia ya bonde la mto Ruaha mkuu waligundua uharibifu huo wa kimazingira na pamoja na kuwapiga faini ya shilingi milioni 10 kutokana na kulima mahindi na migomba ndani ya hifadhi ya mto na waliwataka kuondoa mazao hayo yaliyolimwa ndani ya mita 60.

Wakili Kongola alizitaka mamlaka za serikali za mitaa kusimamia sheria ya Mazingira ya mwaka 2004 kwa sababu ipo wazi. Alisema kuwa usimamiaji makini wa sheria hiyo utasaidia kudhibiti shughuli za kibinadamu zinazofanyika ndani ya mita 60 katika nyanzo vya maji jambo linalohatarisha uendelevu wa vyanzo hivyo wilayani Kilolo.

Ikumbukwe kuwa shamba la mifugo la Tommy diaries lilipigwa faini ya shilingi milioni 10 kutokana na kulima mahindi na migomba ndani mita 60 kutoka ukingo wa mto Ruaha. Vilevile, shamba la mifugo la Ndoto pia lilipigwa faini ya shilingi milioni 10 kutokana na kufanya biashara bila kuwa na cheti cha tathmini ya Mazingira (EIA).
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...