Jumanne, 27 Juni 2017

BENKI YA NMB YABORESHA HUDUMA KWA WATUMISHI WA UMMA



Na. Mwandishi Maalum, Kilolo

Benki ya NMB imeboresha huduma zake ili kuwanufaisha watumishi wa serikali na sekta binafsi wilayani Kilolo.

Kauli hiyo ilitolewa na Meneja wa benki ya NMB wilaya ya Kilolo, Mary Ngallawa alipowasilisha mada ya umuhimu wa benki ya NMB kwa watumishi wa umma katika maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma iliyofanyika katika Ofisi ya mkuu wa wilaya ya Kilolo wiki iliyopita.

Ngallawa alisema kuwa benki yake imeboresha huduma zake na kuingiza sokoni huduma mpya ili kuwanufaisha wateja wake. Alisema “kutokana na wateja wetu kuwa na majukumu mengi, sasa kwa kutumia simu yako ya mkononi unaweza kuhamisha kiasi cha shilingi milioni tatu kwenda akaunti ya benki yoyote na shilingi milioni tano kwenda benki ya NMB kwa benki ya NMB” alisema Ngallawa. 

Aliongeza kuwa benki yake ina mikopo kwa ajili ya wastaafu wanaopata pensheni kila mwezi. “Lengo la mikopo hii ni kuhakikisha wastaafu wanaendelea kunufaika na huduma za benki yetu kama walivyokuwa katika utumishi wao awali” alisisitiza Ngallawa.

Nae Afisa Mikopo, Benjamini Mwakibete alisema kuwa benki ya NMB inatoa mikopo ya nyumba kwa riba nafuu ya asilimia 19 inayohusisha bima ya nyumba na maisha. Alisema kuwa mikopo hiyo inajumuisha kununua nyumba, kumalizia ujenzi wa nyumba, au kufanya ukarabati wa nyumba iliyokwisha jengwa. Alisema mikopo hiyo ni muhimu wa mtumishi kwa sababu mtumishi ana stahili kuishi katika nyumba nzuri na yenye staha. 

Aliongeza kuwa mtumishi anaweza kupata mkopo kwa ajili ya kununua nyumba toka mashirika yanayojenga nyumba na kuuza kwa wafanyakazi.

Mwakibete alisema kuwa mikopo ya nyumba inayotolewa inaanzia shilingi milioni 10-700,000,000 na inalipwa kwa mwaka mmoja hadi miaka 15. Alisema ili kunufaika na mikopo ya nyumba, lazima mkopaji awe na asilimia 10 ya thamani ya kununua nyumba hiyo na kiasi kinachobaki benki ndiyo itamkopesha mtumishi kupitia shirika la nyumba.

=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...