Jumanne, 27 Juni 2017

HOSPITALI YA RUFAA YATAKIWA KUFANYA KAZI KWA MAADILI NA WELEDI



Na. Mwandishi Maalum, Iringa
Watumishi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa wametakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na weledi wa taaluma zao katika kuhudumia wagonjwa.

Wito huo ulitolewa na Katibu Tawala msaidizi, Sehemu ya Rasilimali watu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Lucas Kambelenje alipokuwa akiongea na watumishi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa katika wiki ya Utumishi wa Umma mkoani Iringa.
 
Katibu Tawala Msaidizi- Utawala, Lucas Kambelenje akiongea na Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa. Kulia ni Mganga Mfawidi na kushoto ni Katibu wa Afya
Kambelenje alisema kuwa watumishi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa wanatakiwa kuwa mfano mzuri katika utoaji wa huduma za afya na tiba. Alisema kuwa hospitali hiyo ili iwe mfano mzuri katika utoaji huduma, lazima watumishi wafanye kazi kwa kuzingatia maadili na weledi wa taaluma zao katika kutoa huduma. Alisema kuwa wananchi wanaoenda kapata huduma hospitalini hapo wanamatarajio makubwa ya kupatiwa huduma bora hivyo, huduma bora na kauli njema zinawapunguzia machungu wanayokuwa nayo hata kabla ya tiba. Alisema kuwa maadili mema kwa mtumishi wa umma ndiyo msingi wa ufanisi katika kazi wanazofanya.

Akielezea mafunzo kwa watumishi wa umma, Afisa Tawala Mwandamizi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Neema Mwaipopo alisema kuwa mwajili ana utaratibu wa kuwapeleka watumishi wake katika mafunzo ili kuongeza ujuzi na pia kuimarisha ujuzi walionao kwa ajili ya kuongeza ufanisi na tija katika utendaji wao wa kazi. 

Ili watumishi waweze kupelekwa katika mafunzo mbalimbali ni lazima taasisi iwe na mpango wa mafunzo kwa mwaka wa fedha husika. Mpango wa mafunzo unategemea na mahitaji halisi ya taasisi. Hivyo, mtumishi hawezi kwenda katika mafunzo kama hayupo katika mpango wa mafunzo” alisisitiza Mwaipopo.
 
Afisa Tawala Mwandamizi, Neema Mwaipopo
Mwaipopo aliongeza kuwa mpango wa mafunzo ni muhimu kwa mwajili kwa sababu unasaidia kufahamu idadi ya watumishi wanaotakiwa kupelekwa katika mafunzo na gharama za mafunzo husika. Alizitaja aina za mafunzo kuwa ni mafunzo ya muda mrefu kama shahada ya kwanza na shahada ya uzamili, mafunzo ya muda wa kati kama stashahada na astashahada, na mafunzo ya muda mfupi.

Wiki ya utumishi wa umma ilianza kuathimishwa tangu tarehe 16-23/6/217 ikiongozwa na kaulimbiu isemayo ‘kuimarisha ushirikishwaji wa jamii katika utoaji huduma: vijana washirikishwe kuleta mabadiliko barani Afrika’.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...