Jumanne, 27 Juni 2017

RS IRINGA YATOA ZAWADI KWA MAKAO YA WATOTO ILALA



Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Iringa imekabidhi zawadi za sherehe ya Eid El Fitri kwa makao ya watoto ya Dar-bilaal & Dar-fatma.

Zawadi hizo zilikabidhiwa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza katika makao ya watoto yaliyopo eneo la Ilala mjini Iringa.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza akikabidhi zawadi za Eid El Fitri

Masenza alisema kuwa ofisi yake inatambua kuwa jukumu la malezi ya watoto walio katika mazingira magumu si jukumu la taasisi ya Dhi Nureyn pekee bali jukumu la jamii nzima. Aidha, alitoa rai kwa jamii nzima kuwasaidia watoto wanaolelewa katika makao ya watoto yaliyopo mkoani Iringa.  
Zawadi zilizotolewa na Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Iringa ni mchele kilo 150, mbuzi mmoja, sabuni katoni tano na mifuko mitano ya peremende.

Mkuu wa makao hayo ya watoto Ally Hassan alishukuru kutembelewa na mkuu wa mkoa na katibu tawala mkoa na zawadi walizopatiwa. Alisema kuwa kutokana na zawadi hizo watoto hao watasherehekea vizuri sikukuu ya Eid el Fitri.

=30=


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...