Jumatatu, 17 Julai 2017

CGF AOMBWA TENKI LA MAJI GARI LA ZIMAMOTO



Na. Mwandishi Maalum, Iringa
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji nchini ameombwa kuangalia uwezekano wa kubadilisha tenki la maji kutoka katika magari ya Zimamoto ambayo hayafanyi kazi ili lihamishiwe katika gari lililopata ajali mkoani Iringa kuendelea kutoa huduma.

Ombi hilo lilitolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akishukuru baada ya kukabidhiwa msaada wa gari la Zimamoto na uokoaji kutoka kwa mdau wa maendeleo katika mkoa wa Iringa, Zacharia HansPope katika kituo cha Zimamoto na uokoaji mjini Iringa.
 
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza (kushoto) na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye (kulia) wakiteta jambo
Masenza alisema “kwa kuwa gari lililopata ajali limeharibika tenki la kuhifadhia maji, nikuombe uangalie uwezekano wa kuhamisha tenki kwenye magari yako yaliyopaki ili lije kufanya kazi mkoani Iringa”. Alisema kuwa upatikanaji wa tenki hilo utasaidia gari lililopata ajali kuanza kufanya kazi tena kwa gharama nafuu zaidi.

Mkuu wa mkoa aliwataka wakazi wa Iringa kuiga mfano nzuri wa Zacharia HansPope wa utayari wa kuchangia shughuli za maendeleo kwa mkoa wa Iringa.

Wakati huohuo Mkuu wa Mkoa wa Iringa alipongeza utendaji kazi wa Kamanda wa Zimamoto mkoa wa Iringa, Mrakibu kennedy Komba. “Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji Mkoa wa Iringa ni mtu makini katika utendaji wake, amekuwa akinipa ushirikiano sana, pia yupo haraka katika utoaji wa Taarifa na kuchukua hatua sahihi” alisema mkuu wa Mkoa.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...